MwanzoContactsEmail
Home Michezo Kandanda Yanga yahofia usalama Misri
BOOKMARK THIS PAGE
Yanga yahofia usalama Misri  Send to a friend
Saturday, 04 February 2012 09:12

Kalunde Jamal
UONGOZI wa timu ya Yanga umesema hali ya machafuko iliyotokea nchini Misri inatishia amani na kuvitaka vyombo husika kuhakikisha ulinzi wa kutosha unakuwapo watakapokwenda kucheza na Zamalek baadaye mwezi huu.
Yanga itacheza na Zamalek katika mechi ya raundi ya kwanza ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Februari 18 mwaka huu mjini Cairo.

Akiongea na Mwananchi jana, Katibu Mkuu wa Yanga, Selestine Mwesigwa alisema kuwa hali ya usalama wa viwanja nchini humo si shwari kutokana udhaifu katika ulinzi.

"Usalama ni mdogo, tunaliomba Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kufuatilia kwa karibu hali ya usalama nchini humo kabla ya sisi kwenda kucheza," alisema Mwesigwa.

Anasema amefurahishwa na hatua ya TFF ya kushtushwa na jambo hilo, lakini imewataka wasiishie kushitushwa tu bali wachukue hatua kwa kuonyesha vitendo.

Mwesigwa alisema hata kabla ya maafa hayo, hali ya usalama kwenye viwanja vingi nchini Misri si shwari na kukumbushia mechi waliyocheza miaka ya nyuma dhidi ya Al Ahli ilibidi ulinzi kuongezwa.

"Nashukuru mechi ya kwanza itakuwa nyumbani, hofu yetu ni mechi ya marudiano itakayochezwa ugenini. TFF ishirikiana na Shirikisho la soka Afrika (CAF) kuhakikisha kunakuwapo na ulinzi wa kutosha," alisema Mwesigwa.

Juzi usiku zaidi ya mashabiki 74 waliuawa wakati wa vurugu za mashabiki kwenye Uwanja wa Port Said wakati wa mechi iliyozikutanisha timu za  Al Ahly na Al-Masry.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #1 2012-02-04 09:50
Yanga kuweni makini sana na suala hili tusije kuwakosa akina Niyonzima,kanav arro,kiiza(Dieg o)
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner