
| Kumekucha Ligi Daraja la kwanza | Send to a friend |
| Saturday, 04 February 2012 09:15 |
|
Jessca Nangawe Akitangaza ratiba hiyo Afisa habari wa Shirikisho la soka Tanzania TFF, Boniface Wambura alisema katika Kundi A, Morani FC itakuwa mwenyeji wa Burkina Faso ya Morogoro katika mchezo utakaochezwa Kiteto mkoani Manyara huku kwa upande wa Kundi B timu zote sita zitakuwa uwanjani. Kwa upande mwingine Wambura alisema timu ya Small Kids ya Rukwa itacheza na Polisi ya Iringa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, Mbeya City na Tanzania Prisons zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya na Majimaji na Mlale JKT watapepetana katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea. Kundi C litaanza kwa mechi mbili ambapo AFC ya Arusha watakuwa wageni wa Manyoni mkoani Singida na Rhino na Polisi Tabora zitakwaruzana kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora. Mechi nyingine ya kundi hilo itakuwa kati ya 94 KJ na Polisi Morogoro itachezwa kesho kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi Mkoani Pwani. "Timu zote tayari zimejiandaa kuanza kwa ligi hiyo na tayari zimewasili katika mikoa yao na baadaye timu tisa zitasonga mbele kwenye ligi ndogo ya kupata timu tatu zitakazopanda Ligi Kuu msimu ujao," alisema Wambura. |














