
| Barca majeruhi kibao | Send to a friend |
| Saturday, 28 January 2012 09:21 |
|
BARCELONA, Hispania Hii ina maana, Barca watashuka kwenye Uwanja wa El Madrigal bila wachezaji sita akiwamo David Villa, Ibrahim Afellay na Andreu Fontas, ambao tayari ni majeruhi, huku Seydou Keita akiwa na timu ya taifa kwenye michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.Lakini pia imethibishwa kuwa Iniesta ana matatizo ya misuli na huenda akawa nje ya uwanja kwa muda wa wiki tatu. "Kwa sasa, hatuna wachezaji wengi, lakini ni lazima tusonge mbele," alisema Pep Guardiola. Timu hiyo ilisogea juu kidogo ya mstari wa hatari kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Sporting Gijon, huku kiungo mkongwe Marcos Senna akijiandaa kuikabili vilivyo Barca.Katika mechi nyingine, Atletico Madrid ambayo imekuwa na mwanzo mzuri tangu kujiunga kwa Diego Simeone, itakuwa nyumbani kwa Osasuna. "Ni lazima tuifikirie mechi dhidi ya Osasuna kwa sababu tumepita kwenye wakati mgumu na sasa tunaendelea kuonyesha kiwango kizuri, muhimu ni kutorejea tena nyuma," alisema Simeone. "Osasuna ni timu ngumu lazima tucheze kwa kujiamini na kupata ushindi ili tuendeleze mwanzo mzuri." Valencia, wakiwa kwenye nafasi ya tatu watakumbana na Racing Santander wakitarajia kuendeleza pengo lao la pointi nne dhidi ya Levante watakaokuwa nyumbani kwa Getafe. Espanyol, katika nafasi ya tano watakuwa na mshikeshike dhidi ya Real Mallorca katika mechi itakayochezwa leo. |













