
| Man United yaikamata Man City kileleni | Send to a friend |
| Thursday, 02 February 2012 08:13 |
|
LONDON, England Shujaa wa Everton kwenye Uwanja wa Goodison Park alikuwa mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Darron Gibson aliyefunga bao pekee kwenye mechi hiyo. City walicheza vizuri kipindi cha kwanza kwa kufanya mashambulizi ya mara kwa mara, huku mshambuliaji Samir Nasri akishindwa kufunga baada ya shuti lake kugonga mwamba. Kulikuwa na tukio la shabiki kuvamia uwanjani na kwenda kwenye lango la kipa Joe Hart kabla watu wa usalama kwenda kutoa na kusababisha mpira kusimama kwa dakika nne mwishoni mwa kipindi cha kwanza. Gibson alifunga hilo kwa shuti kali akiwa umbali wa mita 20 lililombabatiza Gareth Barry na kujaa wavuni. Manchester United ilirejea kwa kishindo toka kuondolewa kwenye michuano ya Kombe la FA na juzi usiku walitumia vizuri Uwanja wao wa Old Trafford kuifunga Stoke City. Katika mechi hiyo, United haikucheza vizuri pamoja na kuibuka na ushindi, huku ikifunga bao la kwanza likifungwa kwa mkwaju wa penalti na mshambuliaji Javier Hernandez. Penalti hiyo ilitolewa baada ya Jermaine Pennant kumchezea vibaya Park Ji-sung ndani ya eneo la hatari. Gareth Bale alikuwa wa kwanza kuziona nyavu za Wigan baada ya kupokea pasi ya Luka Modric na kuukwamisha wavuni mpira, kabla ya muda mfupi baadaye Modric kuongeza bao la pili akifunga kwa shuti kali la mita 20. Goli la kujifunga mwenyewe la mchezaji Neil Taylor katika sekunde za majeruhi, lilitosha kuzipa sare ya bao 1-1 Chelsea na Swansea kwenye Uwanja wa Liberty. Mchezaji wa zamani wa Chelsea, Scott Sinclair alikuwa wa kwanza kufunga bao kwa Swansea kabla ya bao la kujifunga wenyewe Taylor.Katika mechi hiyo, Chelsea walilazimika kucheza pungufu baada ya Ashley Cole kuonyesha kadi ya pili ya njano kwa kosa la kumchezea vibaya Nathan Dyer. Hata hivyo walicheza kwa nguvu na kufanikiwa kusawazisha bao baada ya mkwaju mkali wa Jose Bosingwa kumbabatiza Taylor na kujaa wavuni zikiwa zimesalia sekunde tu mchezo kumalizika. Liverpool nayo ilipata ushindi wa pili katika mechi saba baada ya kuifunga Wolves mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Molineux. Mchezaji Andy Carroll alikufunga bao lake la kwanza Ligi Kuu tangu ajiunge na Liverpool Januari mwaka jana. |














