MwanzoContactsEmail
Home Michezo Michezo ya Kimataifa Zidane aitwa kuiokoa Ufaransa
BOOKMARK THIS PAGE
Zidane aitwa kuiokoa Ufaransa  Send to a friend
Thursday, 02 September 2010 21:37

CLAIREFONTAINE, Ufaransa
KIUNGO wa zamani wa Ufaransa, Zinedine Zidane juzi aliunganisha nguvu na kocha, Laurent Blanc kujenga morali ya wachezaji iliyopotea baada ya Fainali za Kombe la Dunia mwaka huu.

Zidane alikutana na wachezaji kwenye mji wa Clairefontaine na walikuwa wakiangalia mkanda jinsi Ufaransa ilivyotwaa Kombe la Dunia 1998 na lile la Ulaya 2000.

Ufaransa itacheza na Belarus leo kabla ya kwenda Bosnia Jumanne kwa ajili ya mechi za kufuzu Euro 2012.

“Nawatakia kila la kheri katika siku za kwanza za maandalizi yao,” alisema Zidane, ambaye aliwatembelea Clairefontaine kwa mara ya mwisho walipokuwa wakijiandaa kwa Fainali za  2006.

“Ni wachezaji wapya, wazuri wanaoweza kutuunganisha lakini inatakiwa wajitambue na watambue majukumu yao ya uwanjani.”

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner