MwanzoContactsEmail
Home Jumapili Habari Wahadzabe wapewa elimu ya kupiga kura
BOOKMARK THIS PAGE
Wahadzabe wapewa elimu ya kupiga kura  Send to a friend
Saturday, 28 August 2010 19:50

Musssa Juma, Mbulu
 SERIKALI wilayani Mbulu mkoani Manyara, imeanza kutoa elimu ya   ya uraia kwa jamii ya Wahadzabe   wanaoishi katika bonde la Yaeda ili wajitokeze kwa wingi kwenye kampeni na kupiga kura katika uchaguzi mkuu ujao.
 
Mkuu wa wilaya ya Mbulu, Anatory Choya akizungumza na mwananchi mjini hapa, alisema jamii ya wahadzabe, moja ya jamii zinazoishi maisha ya asili hapa nchini, imewekewa utaratibu mzuri wa kushiriki kwenye uchaguzi.
 
"Tayari elimu imeanza kutolewa na kuna baadhi yao walishiriki hata katika kura za maoni, hivyo tumejipanga kuhakikisha wanashiriki katika uchaguzi kama walivyo raia wengine," alisema Choya.
 
Alisema sambamba na kushiriki katika uchaguzi huo, pia elimu bado inatolewa ili jamii hiyo iweze kukabiliana na changamoto mbali mbali za kiuchumi ikiwepo kupata elimu, chakula na makazi bora.
 
"Tatizo lililopo ni kwamba kuna baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo hayataki jamii hii ibadilike kwani yananufaika kutokana na hali ya jamii hii"alisema Choya.
 

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
  • Kupiga Kura

  • Jumapili


Ajali ya Meli ZnZ inatufundisha nini?