MwanzoContactsEmail
Home Jumapili Biashara Tambaza ya Sekondari kukarabatiwa
BOOKMARK THIS PAGE
Tambaza ya Sekondari kukarabatiwa  Send to a friend
Sunday, 29 January 2012 10:22

Nora Damian
SERIKALI imetoa Sh100 milioni k ukarabati Sekondari ya Tambaza kutokana na majengo mengi ya shule hiyo kuchakaa.Ukarabati huo ambao tayari umeanza utahusisha vyoo vya wanafunzi, maabara ya fizikia na kemia, madarasa 28 na mfumo wa umeme.

 Akizungumza Dar es Salaam jana, kwenye mahafali ya kidato cha sita, Mkuu wa shule hiyo, Hussein Zubeir, alisema shule hiyo ni kati ya shule kongwe nchini iliyofunguliwa mwaka 1957 na sasa inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo uchakavu wa majengo.

Zubeir alitaja changamoto nyingine zinazowakabili kuwa, ni upungufu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ukosefu wa uzio wa uhakika na usafiri kwa wanafunzi.Nyingine ni upungufu wa walimu kwa baadhi ya masomo, uchakavu wa jengo la utawala na nyumba za walimu na viwanja vya michezo.

“Tunaomba tupatiwe walimu hasa wa masomo ya sayansi na hisabati, ili kuukabili uhaba wa walimu,” alisema Zubeir.Pia, mkuu huyo wa shule aliitaka Serikali kuendelea kuboresha mishahara na maslahi ya walimu, ili kukabiliana na uhaba wa walimu kutokana na wengi kuhama shule au kwenda kwenye shughuli zinazolipa zaidi.

Akisoma risala ya wahitimu, Caroline Yesse, alisema kukosekana kwa vitabu vya kutosha kunarudisha nyuma jitihada za wanafunzi kujisomea.Katika mahafali hayo zaidi ya wanafunzi 500 walihitimu kidato cha sita.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #1 2012-04-02 01:37
et tmbza kna hostel apo
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner