MwanzoContactsEmail
Home Jumapili Biashara Songea yapima viwanja 10,000
BOOKMARK THIS PAGE
Songea yapima viwanja 10,000  Send to a friend
Sunday, 05 February 2012 10:03

Joyce Joliga,Songea
ZAIDI ya viwanja 10,000 vya makazi katika Kata ya Mshangano Manispaa ya Songea  vimepimwa hadi sasa na Kampuni ya Ardhi Plan limited ya jijini Dar es Salaam kupitia mradi wa upimaji viwanja  ulioibuliwa na wananchi wenyewe.

Akizungumza na gazeti hili  jana Mwenyekiti wa Mtaa wa Mshangano, Paulo Mangwe alisema mradi huo umekubalika na Wananchi wanaotaka viwanja vyao vipimwe ili kuondokana na makazi holela huku mradi ukitarajia kukamilika Februari mwaka huu.

Mangwe alisema kuwa hadi sasa tayari michoro 23 inafanyiwa kazi na kwamba hakuna matatizo yaliyojitokeaza kwa kuwa wananchi wanatoa ushirikiano wakionyesha kuridhishwa na kazi inayoendelea.

 “Hadi sasa kazi ya upimaji wa viwanja inaendelea vizuri na tayari viwanja 10,000 vimeshapimwa na wananchi wengi wamepata ajira kupitia mradi huo. Tunatarajia ajira zitaongezeka  kwa  wananchi ,” alisema Mangwe
Mwenyekiti huyo alifafanua kuwa kazi hiyo inafanikiwa kutokana na Kamati ya Upimaji kushinda maeneo ya kazi kusaidia kuwapa wananchi maelekezo wanapopata shida ya kuelewa.

Alitoa ushauri kwa kata nyingine na halmashauri nyingine kutumia kampuni kupima viwanja ili kupunguza migogoro ya wanananchi kuuziwa kiwanja kimoja mara mbili.

Alisema upimaji huo wa viwanja utasaidia wananchi kupata makazi bora, kwa kuwa thamani ya ardhi yao inapanda kutoka mashamba hadi viwanja, hivyo kuweza kupata Benki za Ardhi.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner