
| Tarangile watakiwa kuanzisha hifadhi za jamii | Send to a friend |
| Sunday, 05 February 2012 10:03 |
|
WANANCHI wa vijiji 45 vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Tarangire vimetakiwa kuanzisha Hifadhi za Jamii za Wanyamapori(WMA), ili waweze kunufaika mapato yatokanayo na sekta ya utalii. Mhifadhi Utalii wa Hifadhi ya Taifa ya Tarangire, Beatrice Kessy alisema hayo mbele ya wanahabari, akieleza kuwa kwa sasa vijiji hivyo havinufaiki ipasavyo na wanyamapori waliopo katika maeneo yao hasa wakati wa masika. Kessy alisema kuwa kuanzishwa kwa WMA katika vijiji hivyo vya Wilaya za Simanjiro, Monduli, Babati, Kondoa na Kiteto kutasaidia pia kupunguza ujangili wa wanyamapari Alisema kuwa hifadhi hiyo tayari imeanza kuwasaidia baadhi ya viongozi wa mila na vijiji kutembelea maeneo ambayo WMA zimeanzishwa na kuwa na manufaa makubwa. "Tunawapeleka WMA wa Burunge na Longido ili kujionea wenzao ambao wamenufaika kwani wanapokea fedha za watalii wanaowatembelea, fedha za kuwekwa mahema na fedha na ujenzi wa mahoteli katika maeneo yao,"alisema Kessey Awali Mhifadhi Mkuu wa Tarangire,Erastus Lufungulo alisema kuwa umuhimu wa kuwa na WMA katika vijiji hivyo ni mkubwa kwani karibu vyote vipo katika maeneo ya mapito ya wanyama na ukanda wa wanyama. "Hili ni eneo la kilomita 30,000 za mraba, lote wanyama wanazunguka na wakati wa kiangazi ndipo wanyama wengi hurudi ndani ya hifadhi ambapo kuna Mto Tarangire usiokauka maji,"alisema Lufungulo. Hifadhi ya Taifa ya Tarangire ina ukubwa wa kilometa 2850 za mraba ambapo inapakana na Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara. |

Habari Mpya
Picha
Zenye Mvuto
- Nafasi za Kazi
- Links za wateja na washirika wetu
- Muswada wa madini waitoa jasho serikali
- Bi kizee asafari kilometa 50 kupinga hotuba ya JK, AMUONYA ASITUMIE MADARAKA YAKE VIBAYA
- Mishahara sekta binafsi Tucta yashtukia danganya toto
- Vigogo UVCCM wajiuzulu
- Mwinyi atetea ajira za wafanyakazi, ashauri utu uheshimiwe kudumisha Amani














