
| Kocha: Messi kukosa penalti siyo 'ishu' | Send to a friend |
| Sunday, 05 February 2012 09:45 |
|
KOCHA wa Barcelona, Pep Guardiola amesema kuwa hakuna mchezaji kama Lionel Messi pamoja na kukosa penalti katika mechi ya timu yake dhidi ya Valencia katikati ya wiki. Mchezaji huyo alishindwa kufunga penalti katika mchezo uliomalizika kwa Barca kutoka sare ya 1-1 na Mestalla ikiwa ni mechi ya kwanza ya Copa del Rey nusu fainali. "Lionel yuko vizuri wakati wote, ni mchezaji mwenye sifa zote," Guardiola aliwaambia waandishi wa habari. " Ana kila aina ya uwezo, na amefanya mengi na hilo halina ubishi. "Bila kuwa katika kiwango chake, bado ni mzuri kwa wachezaji wengine. Wakati mwingine huvaa majukumu ya mwingine uwanjani. Linapokuja suala la penalti, hutokea mambo kama hayo. Natumai ataendeleza rekodi yake nzuri. "Kilichotokea, ukweli ni kwamba kimetuharibia. Tuko kwa ajili ya kumsaidia, na tunafahamu kuwa anahitaji kusaidiwa. Kila mmoja anafurahi kuona Messi yuko uwanjani." Guardiola alikanusha kusema kuwa timu yake iko kwenye mgomo kwa kile kilichoelezwa kuwa timu yake ilicheza mechi tatu bila ushindi. "Ni ngumu kufahamu timu inakabiliwa na matatizo gani," aliongeza, "Nitafurahi tu karibuni. Katika mechi dhidi ya Valencia hatukuwachezesha Xavi, [Andres] Iniesta, [David] Villa au [Daniel] Alves, ambao ni roho ya timu. "Tulikuwa tunajaribu wengine. Karibu mambo yatakuwa mazuri." Barca iko nyuma kwa pointi saba na Real Madrid. |
| Last Updated on Sunday, 05 February 2012 10:13 |

Habari Mpya
Picha
Zenye Mvuto
- Nafasi za Kazi
- Links za wateja na washirika wetu
- Muswada wa madini waitoa jasho serikali
- Bi kizee asafari kilometa 50 kupinga hotuba ya JK, AMUONYA ASITUMIE MADARAKA YAKE VIBAYA
- Mishahara sekta binafsi Tucta yashtukia danganya toto
- Vigogo UVCCM wajiuzulu
- Mwinyi atetea ajira za wafanyakazi, ashauri utu uheshimiwe kudumisha Amani














