
| Wachezaji, viongozi CDA wasimamishwa | Send to a friend |
| Sunday, 05 February 2012 09:46 |
|
Masoud Masasi, Dodoma Timu hiyo ambayo inahaha kupanda daraja, ilifanya kitendo kisicho cha kiungwana hivi karibuni baada ya kumvamia mwamuzi Kimu Rajab mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo na kuanza kumshambulia kwa kile kilichoelezwa aliwapendelea wapinzani wao. Katibu wa Dorefa, Aboubakar Ibrahim alisema kuwa kamati ya mashindano iliyokaa juzi ambayo ilipitia taarifa ya msimamizi wa mchezo na mwamuzi huyo imeamua kuwafungia mechi tatu wachezaji na viongozi wao. Ibrahim aliwataja wachezaji hao kuwa ni Aron Michael na Tamimu Abdul amao pia wametozwa faini ya Sh50,000 kila mmoja huku kwa upande wa makocha hao Mrisho Songa na Juma Ikava wakitozwa Sh60,000 kila mmoja. Alisema kwa upande wa waamuzi kamati hiyo imetoa onyo kali kwa Shukuru Said, Omari Juma na Linyasi Saidi kutokana na kutokuwa makini uwanjani na kutakiwa kuongeza umakini wanapokuwa kwenye mechi. |
| Last Updated on Sunday, 05 February 2012 09:53 |

Habari Mpya
Picha
Zenye Mvuto
- Nafasi za Kazi
- Links za wateja na washirika wetu
- Muswada wa madini waitoa jasho serikali
- Bi kizee asafari kilometa 50 kupinga hotuba ya JK, AMUONYA ASITUMIE MADARAKA YAKE VIBAYA
- Mishahara sekta binafsi Tucta yashtukia danganya toto
- Vigogo UVCCM wajiuzulu
- Mwinyi atetea ajira za wafanyakazi, ashauri utu uheshimiwe kudumisha Amani














