MwanzoContactsEmail
Home Jumapili Michezo Ghana, Tunisia kusaka tiketi leo
BOOKMARK THIS PAGE
Ghana, Tunisia kusaka tiketi leo  Send to a friend
Sunday, 05 February 2012 09:48

BATA, Equatorial Guinea
KIU ya Ghana kusubiri miaka 30 kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika, leo inakumbana na changamoto kubwa pale itakaposhuka dimbani kuvaa na Tunisia katika mechi ya robo fainali ya michuano hiyo.

Mshindi wa mechi hiyo atakumbana na mshindi wa robo fainali nyingine kati ya Zambia na Sudan watakaopambana Jumatano ijayo mjini Bata, Equatorial Guinea.

Ghana (Black Stars) ilifikia hatua hiyo baada ya kuifunga Botswana bao 1-0 katika mechi ya ufunguzi wa michuano hiyo, na kisha kuifunga Mali mabao 2-0, kabla ya kwenda sare ya 1-1 na Guinea katika mechi ya mwisho ya Kundi D.

Kocha wa Ghana, Goran Stevanovic, aliyetoa ahadi ya kutwaa ubingwa wa michuano hiyo hapo Februari 12, amesema kikosi chake kitacheza vizuri.

Kiungo anayecheza soka la kulipwa, Ukraine Derek Boateng, yeye alisema wazi kuwa mechi ya leo ni mtihani mkubwa kwao. "Tunisia wana timu nzuri. Wana nidhamu kubwa uwanjani kama ilivyo kwa Guinea," alisema Boateng, ambaye alicheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Guinea.

"Tunafahamu mchezo utakuwa mgumu, lakini ni matarajio yetu tutafanya kila linalowezekana kushinda na kwenda nusu fainali."

Nahodha wa zamani wa Ghana, Sammy Kuffour alisema kikosi chao ni lazima kiwe makini kumkaba mshambuliaji hatari wa Tunisia, Youssef Msakni aliyefunga bao nzuri dhidi ya Morocco.

"Ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa uwanjani, lazima macho yawe kwake muda wote wa mchezo," alisema Kuffour.

"Labda kocha atampanga mtu maalum wa kumchunga kama alivyofanya wakati tukicheza na Mali Seydou Keita kupewa ulinzi mkubwa."

Nahodha John Mensah amepata nafuu baada ya kuumia misuli.

Tunisia inaonekana kuwa mshindani wa kweli wa Ghana baada ya kupita Kundi C ambalo lilimaliza mechi, huku wenyeji Gabon wakishika nafasi ya kwanza. Timu zingine ni Morocco na Niger.

Tunisia (Carthage Eagles) waliotwaa ubingwa wakati walipoandaa fainali za mwaka 2004 ikiwa ni mara ya tatu, waliwafunga Ghana bao 1-0 ilipocheza nayo mara ya mwisho mwaka 2006 katika mechi ya kirafiki ya kimataifa.
Tangu mara ya mwisho ilipotwaa ubingwa mwaka 2004, Tunisia imekuwa tishio kwa vigogo katika michuano hiyo. Mwaka 2006 walitolewa na Nigeria kwa mikwaju ya penalti hatua ya robo fainali na Nigeria.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner