MwanzoContactsEmail
Home Jumapili Michezo Kombe la Taifa kikapu Nov.
BOOKMARK THIS PAGE
Kombe la Taifa kikapu Nov.  Send to a friend
Saturday, 28 August 2010 19:58

Jessca Nangawe
MASHINDANO ya mpira wa kikapu kuwania Kombe la Taifa yamepangwa kufanyika baadaye Novemba mwaka huu yatajumuisha mikoa yote ya Tanzania.

Katibu msaidizi wa Chama cha mpira wa kikapu Tanzania, Michael Maluwe alisema kwa sasa wako katika mchakato wa kutafuta wadhamini wa kusaidi kufanikisha mashindano hayo mapema Novemba.

Maluwe aliiambia Mwananchi Jumapili jana kuwa mpaka sasa hawajapanga tarehe kamili ya kuanza mashindano hayo na wako katika mazungumzo na wadhamini.

Alisema mashindano hayo tayajumuisha mikoa yote ya Tanzania na  lengo kubwa ni kupata wachezaji waliofanya vyema na kuunda timu ya taifa na wengine kuwakilisha mikoa yao katika mashindano mbalimbali ya ndani na je ya nchi.

"Bado tupo katika mchakato wa kupata wadhamini ingawa tayari tumepanga yatafayika Novemba ila tarehe bado hatujapanga kwa sasa...cha msingi tunaiomba mikoa ianza maandalizi yao mapema ya kuandaa mashindano," alisema Maluwe.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
  • Kupiga Kura

  • Jumapili


Ajali ya Meli ZnZ inatufundisha nini?