MwanzoContactsEmail
Home Jumapili Uchambuzi & Maoni Husna hakumudu UWT, anamudu U-DC!
BOOKMARK THIS PAGE
Husna hakumudu UWT, anamudu U-DC!  Send to a friend
Saturday, 01 May 2010 21:24

Na Angetile Osiah
NILIPATWA na mshangao wakati niliposoma mintaarafu ya maisha ya waziri wetu wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Bi Sophia Simba katika mahojiano yake na gazeti la kila wiki la Raia Mwema.
Nilishangaa kwa kuwa sikutegemea kiongozi kama yeye katima karne hii ambayo uongo ndiyo sera, kuwa mkweli kiasi hicho cha kuwa tayari kuanika kila kitu ambacho alidhani watu wanakitafsiri tofauti.


Navyoelewa ni kwamba wengi wangetumia fursa hiyo ya kuweka mambo sawa kwa kuzungumza siasa za ajabu na pengine hata kusingizia kuwa yote mabaya yanayozungumzwa dhidi yake ni uongo na uzushi.
Lakini Simba hakuwa hivyo. Aliamua kuweka hadharani yote ambayo yanazungumzwa vibaya dhidi yake na mengine ambayo yanakaribiana na ukweli, lakini yakizungumzwa kwa njia ambazo zinamchafua mtu.


Isingekuwa rahisi kwa kiongozi kama Simba kueleza bayana kwamba Kitwana Kondo alikuwa "boyfriend" wake, maana hiyo ingetafsiriwa katika picha pana zaidi kwamba kumbe huyo mama alikuwa akisababisha mwanamke mwenzake kukosa usingizi kwa ajili yake!
Lakini pia aliweka bayana kitu ambacho kinaweza kuwa tafsiri mpya ya "boyfriend" maana alikiri bayana kuwa alizaa na Kitwana Kondo mtoto mmoja.


Labda tuachane na mwandani wake. Maana unaweza kujikuta unaingia kwenye kundi ambalo linamuelewa au kumuelezea Simba kwa maneno mabaya.
Labda nizungumzie hili la Husna Mwilima, katibu mteule wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), ambaye hakumudu kufikisha hata mwaka mmoja kutokana na wale wanaotaka kumchafua Waziri Simba kusema "eti" alikuwa na tofauti naye.


Mama Simba akaweka bayana kwamba "akha" hakuwa na tofauti naye kwa sababu yeye ndiye aliyependekeza jina lake na kulipeleka kwenye Baraza la UWT ambalo lilimpitisha kuwa katibu mkuu.
Naona kuwa pengine watu wanaona kuwa Waziri Simba, ambaye ni mwenyekiti wa moja huo, alikuwa na tofauti Husna ni kitendo chake cha kukiri kuwa alifanya makosa kumpendekeza mkuu huyo mpya wa Wilaya ya Tandahimba.
Katika makala hiyo, Waziri Simba anaeleza bayana kuwa alifanya makosa; kwanza kumteua Husna kwa kazi hiyo ambayo ilikuwa kubwa kwake kutokana na kiwango chake cha elimu; na pili kumteua Bi Husna bila ya kumshirikisha mtu mwingine yeyote.


Anaeleza mama huyo kuwa kazi ya katibu mkuu wa UWT ni kubwa sana kulinganisha na kiwango cha elimu cha Husna hivyo asingeweza kuimudu kazi hiyo ambayo iliwahi kufanywa na kina mama wengine wenye uwezo.
Nilimsifu kwamba, aliweza kuweka kile anachoamini kuwa ni ukweli ili kuwaweka sawa wale wanaoona kuwa alikuwa na tofauti na mama huyo.
Mtu anayehusika na utawala bora anapoona kuwa mtu fulani hamudu nafasi fulani, basi anakuwa ameangalia mambo mengi kiasi kwamba mtu mwingine ambaye utatataka umtumie huyo aliyetemwa utalazimika kufanya kazi ya ziada, hasa inapokuwa suala la kushika ofisi ya umma.
UWT ni ya wanachama wa umoja huo tu ambao wanaweza kukubaliana hata mambo ambayo aliye nje anayaona kuwa hayafai. Kwa hiyo kiongozi kwenye jumuiya kama hiyo anatakiwa kuwa makini na utashi wa watu hao waliouweka kwenye katiba na sheria zao ili mambo yaende sawa.


Kwa hiyo ni rahisi zaidi kuongoza kwenye jumuiya kama hiyo kwa sababu utashi wao uko bayana na hauna utata. Lakini kuongoza wilaya ni kitu kigumu sana hasa ikizingatiwa kuwa utashi wa jamii iliyo kwenye wilaya hiyo hutofautiana sana.
Mahitaji ya wilaya ni makubwa zaidi ya mahitaji ya jumuiya moja, hata iwe ya kitaifa. Matazamio ya wakazi wa wilaya ni makubwa zaidi ya yale ya wanachama wa jumuiya.
Na utendaji wa kiongozi wa wilaya ni mgumu kuliko ule wa jumuiya moja.


Sijui Simba aliona ukosefu wa elimu ya kutosha ya Husna ungeathiri zaidi sehemu zaidi kwenye utendaji wake ndani ya UWT, lakini pengine udhaifu aliouona Waziri Simba ndio nguvu yake ya kuongoza wilaya.
Watu tunatofautiana kimtazamo!
Pengine alikuwa sahihi yule aliyesema "when one door is closed, many more are opened". Ndio maana Sophia Simba alipomuona Husna kuwa hana elimu ya kutosha kuwa mtendaji mkuu wa UWT, Rais Kikwete akagundua kuwa ana elimu ya kutosha kuwa mkuu wa wilaya!
Simba alifunga mlango mmoja, mingine kibao ikafunguka!


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #9 2011-10-21 00:34
Jamani huyu mama ni jasiri na mchapa kazi sidhani kama kuna sababu ya msingi yakumsakama kwa maneno yakisiasa,anauc hungu na nnchi yake na anaweza hata kuongoza inchi hii!!
Quote
 
 
0 #8 2011-04-24 17:34
Usishangae ndg mwandishi,uteuz i wowote chini ya CCM ni kujuana na si kusingatia matakwa ya sheria,masilahi ya taifa na uwezo wa mtu,wanalipana fadhila!!!!!!, tukomboe nchi yetu,tuwaondoe..........
Quote
 
 
0 #7 2011-02-28 09:40
kweli asie kwa kuliona hiloyekujua hakudhamini kwa sisi tunaemfahamu Husna katika utendaji wake wa kazi na usemaji wake wa ukweli tunaweza kuamini kwamba kilichomshida UWT ni kusema uongo au kujipendekezape ndekeza yeye daima usimamia kwenye ukweli na ndio maana kazi ya DC anaiweza tunamshukuru Raisi kikwete kwa kuliona hilo
Quote
 
 
0 #6 2010-10-26 02:34
Hapo ndo utajua ccm ni majungu na uongo kwenda mbele. Iwaje asifae uwt afae wilayani? Hapa kuna mawili, either ni mtenda kazi safi kiasi bosi wake uwt hakumpenda au hamnazo ila anajua kulinda vya wakubwa.
Quote
 
 
0 #5 2010-05-14 14:33
Tatizo la watanzania sio wachambuzi, mnakurupuka tu kutoa lawama, Mbona serikali za awamu zote zilikuwa na viongozi waliokuwa na elimu ndogo, nianze kuwatajia kuanzia awamu ya kwanza? Mbona kila anachokifanya kikwete analaumiwa ? Wacheni Roho mbaya..Mna ajenda zenu..lakini watu wameshazijua
Quote
 
 
+1 #4 2010-05-10 10:46
Jamani huyu mtu siyo kwamba alishindwa kazi kilichomshinda ni kazi za ukatibu mkuu wa Umoja wa Wanawake, kazi zile nyingi hazitakiwe kisomo pale ni uhodari wa kuchimbana sasa kama alishindwa hiyo kazi utasema hawezi
UDC mbona huko nyuma alikuwa ni DC na alimudu, acheni Mama wa watu apige mziko si vizuri kuendelea kumsakama.
Quote
 
 
-1 #3 2010-05-10 08:22
hapa hakuna wakulaimiwa isipokuwa bosi wao kikwete aliyejiingiza kwenye malumbano ya taarabu,haoni mbali bwana huyo ni lazima azikwe nao hao wawili kwa sababu zisizo za kielimu wala ufanisi. Ni kweli watu wa karibu yake hawakufanyiwa vetting maana hiyo tabia ya simba ni chafu mbele ya macho ya vijana wa taifa hili, mwenyekiti wa UWT anapamba vyombo vya habari kwa kutuambia juu ya uhuni wake, kumbe ni kweli tunavyosikia vyeo vinatolewa kwa kulala na wakubwa kwenye serikali ya Kikwete, huko kujidai yeye atahakikisha asilimia 50% ya wanawake kuingia bungeni anakutimiza, bahati mbaya hao ndio atakaowajaza wanawake majabali wenye uwezo na sifa hawatapata hizo nafasi hizo ni zake binafsi na wakina Husna, Betty Mkwasa, Sofia Simba na wengine hatutaki kuwataja humu
Quote
 
 
+1 #2 2010-05-05 21:21
khaa
Mimi nashangaa kuona kuwa huyu Husna ndiyo kawa pekee, asiye soma na kapewa madaraka
Tuanzie huko nyuma marehemu diria alikuwa ni form six leaver alikuwa na madaraka ya kila aina
Wengine walikuwa wabunge wa kuteuliwa , mdogo wetu amina chifupi na form six yake ya tambaza sasa wewe aliye kuambia tanzania ni husna mwilima pekee sijui ni nani?
Sisi watoto wa mjini tunamjua kitwana Kondo, huyu akikushika mkono ukwami, sasa mama na uwaziri wko tuambie umesoma wapi mwenzetu?
Quote
 
 
-1 #1 2010-05-05 08:07
Nawaonea huruma wananchi wa wilaya ya Tandahimba, kwani ninavyodhani mie, hawakupaswa kupelekewa mkuu wa wilaya ambaye hamudu kazi. Itakuwa vigumu kuniambia kuwa eti mtu akishindwa ukatibu mkuu wa jumuia eti ataweza ukuu wa wilaya. Hii inadhihirisha ile dhana ya kuwa serikali inaendeshwa kishikaji, inawezekana husna ni mshikaji wa vigogo fulani serikalini ambao wameamua kumtafutia ulaji mshikaji wao baada ya kuona kuwa kibarua chake UWT kimeota nyasi. Peer-Review ni dhana nzuri ya kuona kiongozi anayefaa, sasa kama peers wa husna UWT waliona hafai uongozi inakuwaje anapewa uongozi mwingine. Ndo atamudu uraisi wa wilaya kama kashindwa utendaji wa wilaya? MAKUBWA HAYA. Hongera SOphia SImba kwa kuwa mkweli inabidi watanzania ifike mahali tuambiane ukweli, kama mtu hawezi kazi hawezi tu na ukimbeba kuna siku tu na we unayembeba UTAUMBUKA.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner