MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa Tucta: JK wawajibishe mawaziri wazembe
BOOKMARK THIS PAGE
Tucta: JK wawajibishe mawaziri wazembe  Send to a friend
Monday, 02 January 2012 22:06

Patricia Kimelemeta
SHIRIKISHO la Vyama Vya Wafanyakazi nchini (Tucta), limemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwachukulia hatua viongozi wanaoshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo na kusababisha  kuwepo kwa migogoro ya wafanyakazi nchini.Kauli ya Tucta imekuja siku moja tangu Rais Kikwete adai kwamba anashangazwa na watendaji wanaosababisha kuwepo kwa malimbikizo makubwa ya stahiki ya watumishi wa umma wakiwemo walimu wakati wamekuwa akitoa maagizo ya mara kwa mara juu ya kulipa stahiki zao mapema.

Katibu Mkuu wa Tucta, Nicolaus Mgaya alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa, malimbikizo hayo yanatokana na mawaziri wenye dhamana za Utumishi wa Umma na ile ya Kazi na Ajira kushindwa kutii maagizo ya rais, hivyo kusababisha kuwepo kwa malimbikizo hayo.

Alisema, mawaziri hao walipaswa kuwahimiza watendaji wao ili kuhakikisha stahiki hizo zinalipwa mapema, lakini mpaka sasa wameshindwa kutimiza wajibu.Mgaya alisema mawaziri hao wanapaswa kuwajibishwa kwa kuchukuliwa hatua na mamlaka ya uteuzi ambayo ni rais.

 “Tatizo sio Rais, tatizo liko kwa mawaziri wake, wao ndio wenye jukumu la kuwasimamia watendaji wakuu wa wizara zao ili kuhakikisha kuwa stahiki za watumishi wa Umma wakiwemo walimu zinalipwa kwa wakati ili kuondoa migogoro, lakini mpaka sasa hakuna kinachofanyika zaidi ya maneno,wanapaswa kuwajibishwa,”alisema Mgaya.

Aliongeza malimbikizo ya malipo ya madeni ya walimu na watumishi wengine ni miongoni mwa vichocheo vya migogoro kazini na kwamba uzembe wa watendaji wakuu unapaswa kukemewa kwa nguvu zote.

“Wafanyakazi ni tabaka kubwa nchini na wanachangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa nchi, hivyo wanapaswa kutathiminiwa na kuondoa migogoro,”aliongeza Mgaya.

Hata hivyo Mgaya alisema pamoja na kauli ya Rais Kikwete, Tucta kwa kushirikiana na Chama Cha Walimu(CWT) watahakikisha mgomo wa walimu ulioitishwa wakati shule zitakapofunguliwa unafakiwa ili kilio chao kiweze kufika kwa Rais na kutambua kuwa watendaji wake wanashindwa kuwajibika.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #3 2012-01-04 00:37
Anaestahili kuwajibishwa ni JK kabla ya kuwafikiria wengine. Anajua kuwa anastahili kuwajibishwa kwa utendaji wake mbovu,hivyo hatokuwa na ujasiri wa kumwajibisha fisadi yeyote.Wote waliomzunguka ni watuhumiwa ukianza na yeye mwenyewe.Pigo kubwa kwa Taifa letu Tz,ni kuwa huyu rais bandia ana kama miaka 3 zaidi ya kuiharibu nchi.Ataiacha kwenye hali mbaya kuliko maelezo.Ni heri angeweka record ya kujiuzulu urais na kumwachi mwingine mwenye uwezo wa kuongoza atunusuru,kwa hilo angekumbukwa kuliko kulipeleka taifa mahali hata yeye hajui hatima ya taifa ni nini!Hii post ni kubwa sana kwa mkuu,haiwezi,am ejaribu kutumia mbinu za kujichekesha bila kujua ile post siyo ya kujichekesha.Watu wanataka positive changes na sio ukenuaji kila siku bila maendeleo.Amekenua kwa miaka kama 7 Ikulu lakini hajashtuka kwamba ukenuaji hauna tija kwa taifa.Ona gharasha jingine wizara ya nishati na madini!Huyu mtu sijui aliwezaje kuingia Ikulu,huenda yule marehemu mtabiri wake alichangia kwa kiasi kikubwa kuroga Watz.
Quote
 
 
0 #2 2012-01-03 10:06
kwaTanzania hii ya leo hakuna mwenye uthubutu wakufanya maamuzi magumu'mfumo uliopo serikalini kwasasa niwakulindana na kulipa fadhila ndio maana mambo ya msingi yanaamuliwa kishabiki baada yakuwajibishwa mtu anaachwa astaafu au anapewa LIKIZO BILA MALIPO? TUCTA tuombe tupate katiba mpya haraka itakayo punguza madaraka yarais nakutoa uhuru kwawananchi kusimamia mustakabali wa taifa lao"waelimisheni walio chini yenu watoe maoni Ingawa mchakato wenyewe umetekwa na wasio nadhamira yakweli...
Quote
 
 
0 #1 2012-01-03 07:59
Hapo mie Mwanakijiji nasema Tatizo Kubwa katika Utendaji ni Kiongozi Mkuu.
Anao Mawaziri/Makatibu Wakuu na Wakurugenzi ambao yeye mwenyewe hajui wanachokifanya au kuamua kwa manufaa ya Taifa,hivyo yeye ndio Tatizo katika Ufuatiliaji. Pamoja na kutumia fedha za Uma kwa Semina na vikao vya Uelekezi lakini bado yeye kama mkuu anashindwa kuwa na Uamuzi hata kama nchi i[NENO BAYA]sa waalimu na wataalamu.
Mwanakijiji wa Isanzu-Isene-Iramba.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner