MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa Mgomo wa Tucta kujulikana Juni 5
BOOKMARK THIS PAGE
Mgomo wa Tucta kujulikana Juni 5  Send to a friend
Monday, 31 May 2010 19:41

Patricia Kimelemeta

SHIRIKISHO la vyama vya wafanyakazi nchini (Tucta), linatarajia kutoa tamko la kugoma au kuacha Juni 5, baada ya kukaa kwenye kikao cha majadiliano Juni 4 mwaka huu.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya serikali kushindwa kutoa tamko la makubaliano yao ya kikao cha utatu kilichofanyika Mei 8 mwaka huu, ambapo kwa mujibu wa sheria, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, anapaswa kutoa taarifa ya kikao hicho ndani ya siku 21.

Akizungumza na Mwananchi kwenye mahojiano maalum yaliyofanyika jijini Dar es Salaam jana, Naibu Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholas Mgaya alisema kuwa, kutokana na serikali kushindwa kutoa taarifa yoyote ndani ya siku hizo, baraza linaloratibu mgomo litatoa tamko lake.

Alisema wafanyakazi wamekuwa kimya kutokana na kusubiri tamko la serikali kuhusiana na kikao chao hicho, ambapo mpaka sasa waziri ameshindwa kutoa taarifa yoyote kutokana na hali hiyo watakaa kikao hicho kwa ajili ya kujadili hatua zitakazofuatwa na wafanyakazi hao.

“Tunatarajia kufanya kikao cha mwisho siku ya Ijumaa, ambacho kitatoa mwelekeo  wa wafanyakazi kufanya mgomo au la, kwa sababu tulikuwa tunasubiri tamko la makubaliano kutoka serikalini, lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyika badala yake waziri amekaa kimya,"alisema Mgaya.

Aliongeza kutokana na hali hiyo baraza hilo limesikitishwa na hatua hiyo, kwa  sasa wanaendelea na mikutano ya ndani kwa ajili ya kupanga utaratibu watakaotumia wakati wa kutoa tamko hilo.

Alisema malalamiko ya wafanyakazi juu ya nyongeza ya mishahara ni ya muda mferu, lakini mpaka sasa serikali imeshindwa kuchukua hatua zozote juu ya suala hilo, jambo ambalo linawafanya waamini kuwa wafanyakazi wanadharauliwa.

“Wafanyakazi ndio wanaokuza uchumi wana chi, lakini wanarudishwa nyuma na baadhi ya viongozi kwa kuwadharau na kutosikiliza matatizo yao, jambo ambalo linawafanya waingie kwenye mgogoro mkubwa namna hii na serikali,”anaongeza.

Kwa mujibu wa Mgaya, mbali na tamko hilo pia,siku hiyo hiyo shirikisho hilo litatoa taarifa za kutaka kumshitaki waziri huyo kutokana na kutangaza mishahara yenye mapungufu katika baadhi ya vipengele.

Awali, Tucta ilitoa mapendekezo ya nyongeza ya mishahara baada ya kufanya tathimini na kubaini kuwa, kutokana na hali ngumu ya maisha, wafanyakazi wanalipwa kiasi kidogo.

Tucta ilitoa mapendekezo ya kima cha chini cha mishahara kutoka Sh 84,000 hadi 315,000 kwa mwezi, jambo ambalo serikali imedai kuwa haina uwezo wa kuwalipa.

Mbali na mapendekezo hayo, Tucta imeitaka serikali kupunguza makato ya kodi ya mifuko ya hifadhi ya jamii na kodi.

Kutokana na hali hiyo Tucta ilitangaza mgomo huo ambapo awali ulitakiwa kuanza Mei 5 mwaka huu, baada ya serikali kuwaomba warudi kwenye meza ya majadiliano.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
+1 #4 2010-06-01 19:22
TATIZO VIONGOZI WA TUCTA NI MAJUHA,WALIKOSA BUSARA TOKEA MWANZO, ONA SASA HAWAWEZI KUWASHAWISHI WAFANYAKAZI TENA, USHAURI WA BURE, KAMA UNATAKA KULETA MABADILIKO YEYOTE YA KIMAENDELEO, USICHANGANYE NA SIASA, NA ACHA KUJIKWEZA, UTAAIBIKA KAMA mgaya
Quote
 
 
+1 #3 2010-06-01 17:36
Ombi langu kwenu wafanyakazi kuwajibika zaidi kuleta maendeleo ya nchi yetu,hivyo,kuwa wajibisha hata viongozi wababaishaji kama hawa ghasia na juma kapuya.dunia ya sasa siyo takwimu za mezani tu kudanganya watu miaka hadi miaka.takwimu za kiuchumi duniani pamoja na tz zipo,sasa giliba za nini kwa wafanyakazi? mh kikwete sina imani nawe kabisa.......
Quote
 
 
0 #2 2010-06-01 10:31
Serikali hii haina viongozi wawajibikaji. Tuige mfano kwa wenzetu, mfano, Rais wa Ujerumani amejiuzulu kutokana tu na kauli alizozitoa za kuhusisha ushiriki wa Ujerumani katika vita Afghanistani n.k kwamba ni kwa maslahi ya Ujerumani. Kwa ajili ya kauli tu, Rais anajiuzulu. Tanzania haina uongozi unaojali maslahi na maendeleo ya wananchi wake. Wapo madarakani kwa maslahi yao wenyewe.
Quote
 
 
0 #1 2010-05-31 19:58
Juma Kapuya simwajibikaji,r ais anatakiwa amtimue kazi hana analolifanya nahuyo Hawa Gasia wake mpaka mambo yaharibike ndipo aseme wafanyakazi wanatumiwa na wapinzani
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner