MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa TCU kufanya awamu nyingine ya udahili
BOOKMARK THIS PAGE
TCU kufanya awamu nyingine ya udahili  Send to a friend
Thursday, 30 September 2010 19:33

Hussein Kauli
TUME ya Vyuo Vikuu (TCU) imesema kuanzia wiki ijayo itaanza kupokea awamu ya pili ya maombi ya wanafunzi wanaotaka kujiunga na taasisi za elimu ya juu kwa kutumia mfumo mpya wa udahili wa wanafunzi.

Afisa uhusiano wa tume hiyo, Edward Mkaku aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa kulikuwa na kasoro nyingi kwenye awamu ya kwanza ya udahili na kusababisha waombaji wengi kukosa nafasi.

Alisema baada ya kukamilisha kutoa ya matokeo wanafunzi waliochaguliwa kesho, watafungua tena mitambo ya kudahili wanafunzi kuanzia wiki ijayo ili wanafunzi wenye matatizo waombe upya.  “Siwezi kusema utaanza siku gani na kutakuwa na awamu nyingine zaidi kumaliza matatizo yaliyopo,” alisema Mkaku. Alisema baada ya kumaliza kutoa matokeo yote watatoa majina ya wanafunzi walikosea kwenye maombi yao ili waweze kuomba upya kwa kutumia mfumo huo mpya wa udahili.

Alibainisha kuwa matatizo mengi yaliyotokea yalimesababishwa na wanafunzi kutoelewe vyema mfumo huo, hivyo kufanya maombi yasiyo sahihi kutokana na sababu mbalimbali. “Tatizo la wanafunzi kudahiliwa kwenye kozi ambazo hawakuzichagua limesababishwa na wao wenyewe kutokuwa makini wakati wa kuomba nafasi hizo,” alisema Mkaku.

Alifafanua kwa kuwa kozi ziliwakilishwa na namba za mpangilio (code number), hivyo wako wanafunzi waliochagua namba bila kuangalia inawakilisha kozi gani, matokeo yake wakachagua kozi wasizozitaka.

 “Yupo mwanafunzi alikuja hapa; yeye amefaulu kwa daraja la kwanza nukta nne kwenye mchepuo wa (historia, kiswali na lugha) HKL, lakini aliomba BS in Engineering, na amedahiliwa kwenye kozi hiyo. Sasa huyu hakuwa makini wakati wa kuchagua kozi,” aliongeza Mkaku. 

Aliongeza kuwa wapo wanafunzi walioomba vyuo kwa kutumia mitandao mingine ya simu za mkononi badala ya Vodacom, hivyo maombi yao hayakufika TCU na hivyo kutochaguliwa.

Kutokana na matatizo hayo na mengine, Mkaku alisema bado udahili haujakwisha na aliwataka wanafunzi kusubiri kwani watatoa majina ya wanafunzi waliokosea. “Baada ya kukamilisha kutoa matokeo ya awamu ya kwanza tutafanya uteuzi kwa awamu ya pili na huenda tukafanya uteuzi wa awamu nyingine ili kuhakikisha tunamaliza matatizo yote,” alisema Mkaku.

Kwenye ofisi za TCU juzi, wanafunzi wengi walikuwa wakilalamika kutochaguliwa na wengine kuchaguliwa kwenye kozi ambazo hawakuziomba. “Mimi nimetoka Arusha nimekuja hapa kujua hatma yangu, kwa sababu matokeo yangu ya kidato cha sita yalikuwa mazuri tu lakini sikuchaguliwa na rafiki yangu niliyempita, amechaguliwa kwenye kozi kubwa bila kuliko ufaulu wake,” alisema mwanafunzi aliyejitambulisha kwa jina la Rahim Bendera. Mmoja alidai amekuta jina lake lakini namba siyo yake na mwingine alikuta namba yake, lakini jina la mtu mwingine.    


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #7 2010-10-02 02:54
TCU SHUGHULKIENI SERA NA ITHIBATI YA ELIMU YA JUU. HAYA YA UDAHILI WAACHIENI VYUO WENYEWE NDI MAANA VIMEKUWA VYUO VIKUU. BAADAE MTATAKA MTUNGE MITIHANI, MTOE DIGRII NYIE SASA MNA VURUGU TUPU
Quote
 
 
0 #6 2010-10-02 02:39
NASHAURI TCU WAACHANE NA UDAHILI BADALA YAKE JUKUMU LA UDAHILI LIACHIWE VYUO WENYEWE NA TCU WASHUGHULIKE NA SERA NA ITHIBATI YA ELIMU YA JUU
Quote
 
 
0 #5 2010-10-02 02:36
SUALA LA UDAHILI WAACHIWE VYUO VIKUU. NDIYO MAANA WAKAVIITA AUTONOMOUS (VINAJITEGEMEA) KUWEZA KUDAHILI WANAFUNZI WAKE. ACHENI URASIMU WENU NYIE TCU SHUGHULIKENI NA ITHIBATI YA UBORA WA ELIMU NA SERA. WEWE NKUNYA ACHA MAMBO YAKO YA UDSM WAKATI ULE MIGOMO KIBAO
Quote
 
 
0 #4 2010-10-02 02:32
MFUMO HUU SI MZURI NA SI WA UHAKIKA ZAIDI KWA SABABU UMEONYESHA KUWA NA MAPUNGUFU KIBAO. NAWASHAURI TCU JUKUMU LA UDAHILI WANGEACHIA VYUO WENYEWE NA WAO WASHUGHULIKIE ITHIBATI YA UBORA WA ELIMU NA SERA. HUU NI UBABAISHAJI WA TAASISI HII KUJIPACHIKA MAJUKUMU AMBAYO SI YAKE. HUYU PROF. NKUNYA ANAFAMIKA ENZI ZAKE PALE UDSM KULIKUWA NA MIGOMO KIBAO
Quote
 
 
0 #3 2010-10-01 15:16
tcu endesheni semina ya mfumo huu unavyofanya kazi kwa wenye internet cafe ili wawasaidie vijana waweze jaza vizuri. mbona miradi ya serikali ya ukimwi inamwaga hela nyingi kuelimisha umma kv kwenye mabaa na mahoteli??
Quote
 
 
0 #2 2010-10-01 11:15
MIMI NINAFIKIRI KUNA KASORO NYINGI KATIKA MFUMO HUU MPYA WA UDAHILI WANAFUNZI VYUO VIKUU KWANI KWANZA,HAPAKUWA NA ELIMU ILIYOTOLEWA NA TCU KWA WAHITIMU WOTE KUHUSU UTUMIAJI WA MFUMO HUU MPYA WA UDAHILI.
UNAJUA LAZIMA TUANGALIE NI WATANZANIA WANGAPI WANA UWEZO WA KUPATA TAARIFA KUPITIA MITANDAO KWANI KUNA SEHEMU HATA SIMU HAZIKAMATI NETWORK
KWA HIYO NINAIOMBA SERIKALI IUPITIE HUU MFUMO KWA UPYA.TUSIWE WEPESI WA KUWALAUMU WAHITIMU BILA KUANGALIA NINI KIMEMSIBU.
Quote
 
 
+1 #1 2010-10-01 09:43
katika udahili mara ya kwanza hawakuonyesha kuwa unatakiwa kutuma maombi yako kupitia mtandao wa vodacom lakini gazeti la leo nashangaa kuona kuwa ilitakiwa kutumia mtandao huo hii ina maana gani mbona mnatuyumbisha ? hivyo ingekuwa vizuri kuwaambia wanafunzi mapema kwa vile ilipotokea maombi kutumwa kwenye message basi watu wakatumia mtandao wowote na inawezekana ni wengi maana mimi nilitumia ZAIN kutuma maombi yangu ndiyo maana sikuona jina langu.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner