
| Rostam aponda tiba ya Mchungaji Loliondo | Send to a friend |
| Tuesday, 15 March 2011 21:22 |
|
WAKATI Watanzania wengi wakimiminika kwenda wilayani Loliondo, mkoani Arusha kupata dawa inayodaiwa kutibu magonjwa sugu, Mbunge wa Igunga (CCM), Rostam Aziz ameibuka na kusema tiba hiyo haina lolote akidai kwamba ndugu zake watano wameitumia lakini hawajapona. Akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru wapigakura uliofanyika kwenye Viwanja vya CCM wilayani Igunga, Tabora mbunge huyo alisema haiamini dawa hiyo kwa kuwa ana ushahidi kwa ndugu zake hao ambao anadai kwamba wanaendelea kuugua kisukari licha ya kutumia dawa hiyo siku saba zilizopita. Aliwataka wale watakaokwenda Loliondo ambao wanatumia dawa za hospitalini kuendelea kuzitumia badala ya kuzipuuza na kuzitupa... “Ndugu zangu wananchi wa Igunga, mimi mjomba wangu Hassan mnamfahamu karibu wote hapa mjini ni mgonjwa wa siku nyingi wa kisukari. Ameshakunywa dawa hiyo lakini mpaka sasa ni mgonjwa kama mnavyomuona sasa hiyo dawa inaponyesha nani?” Hata hivyo, aliwataka wananchi wote wenye imani juu ya dawa hiyo waende huku akiwasisitizia kutopuuza ushauri wa madaktari kwani. Wakati Rostam akipinga dawa hiyo, wilayani Kahama, mamia ya wafanyabiashara wamefunga shughuli zao na kukimbilia Loliondo kwa Mchungaji Mwasapile kunywa dawa hiyo huku baadhi ya waliorejea baada ya kuinywa wakidai kuwa hali zao sasa ni nzuri. Wafanyabiashara hao wengi wao wanaondoka kwa siri wakidai wanakwenda Dar es Salaam katika shughuli zao, lakini siri imefichuka baada ya baadhi yao kuoneka katika runinga wakiwa katika foleni wakisubiri kupatiwa huduma hiyo. Mbali ya kuzungumzia suala hilo la tiba ambalo limegusa hisia za wananchi wengi wa Afrika Mashariki, mbunge huyo aliwapa pole wananchi wa Igunga ambao nyumba zao zimeezuliwa na upepo uliosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha wiki iliyopita ambazo ziliathiri kaya 19. Aitoa msaada wa Sh500,000 kwa kila kaya iliyokumbwa na maafa hayo. |

Habari Mpya
Picha
Zenye Mvuto
- Nafasi za Kazi
- Links za wateja na washirika wetu
- Muswada wa madini waitoa jasho serikali
- Bi kizee asafari kilometa 50 kupinga hotuba ya JK, AMUONYA ASITUMIE MADARAKA YAKE VIBAYA
- Mishahara sekta binafsi Tucta yashtukia danganya toto
- Vigogo UVCCM wajiuzulu
- Mwinyi atetea ajira za wafanyakazi, ashauri utu uheshimiwe kudumisha Amani















Comments
rostam kama umesoma masharti manne ya babu utajua kwa nini hukupona na kwa nini hutapona. moja dawa ya babu si sindano ya kudunga ya masaa wala siku saba. dawa ya babu ni IMANI na ukiwa na imani utapona. halafu dawa ya babu ni kwa wasio na usanii kwa watanzania. wapo naweza kukutajia ukitaka ambao babu aliwaambia wakatubu dhambi zao halafu warudi ili awape dawa. labda hakukusemea lolote kwa sababu za usalama wake. ila elewa tu dawa ya babu ni uponyaji kwa imani. kwani ulimpeleka huyo mjomba kwa kakobe? kwa nini? MPELEKE HUYO MGONJWA WAKO KWA MWINGIRA NIMEOTESHWA NI TABIBU WA WAGONJWA WAKO.
Au unaogopa maneno ya Mzee Ndesa wa kuwahimiza wabunge wawasaidie wapiga kura wao kufika kwa Babu?
Mbona rafiki yako wa Monduli amesema dawa ya Babu ni safi?
Hiloooooooo!!!! !!!
Babu alishaonya kuhusu tabia na mienendo yetu kuhusiana na dawa yake. Hao ndugu wa Rostam unategemea 500 zao wamezitoa wapi kama sio kwenye mafungu ya dhuluma ya richmond na dowans. Hela yao haijaswii, kamwe hawawezi kupona. wakitaka kupona, waende mtaani wakafagie barabara, walipwe hela halali kwa kadiri ya jasho lao, then waende tena Loliondo kwa babu na hela hiyo halali, wasipopona basi wana laana ya milele. Adumu Mchngj Ambikile na tiba yake isiyopenda mafisadi
Mwingira nae ana hofu mishemishe zake zitaanguka. Tuwe makini na watu wanaoishi kwa kutegemea sadaka. siku zote wasiwasi wao ni kupoteza wafuasi ambao ndio chanzo cha mapato na migari heavy wanayotembelea.