|
Januari 14, 2006 watu waliosadikiwa kuwa majambazi wauawa
Januari 15, 2006. Zombe atangaza kuua majambazi wanne
Januari 16/17, 2006, Utata waibuka kuwa waliouawa hawakuwa majambazi
Januari 23, 2006 Rais aunda Tume ya Jaji Kipenka kuchunguza mauaji
Januari 24, 2006: Tume yaapishwa na kupewa siku 21 za kufanya kazi.
Februari 17, 2006: Tume yakabidhi taarifa yake kwa Rais Kikwete
Februari 20, 2006: Mwanzo wa kesi askari 11 (bila Zombe)
Juni 9, 2006: Zombe apandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka .
Juni 15, 2006: Zombe afutiwa shtaka la mauaji ya wafanyabiashara hao
Septemba 28, 2006: Washtakiwa wote wapandishwa kizimbani
Mei, 2008: Kesi yaanza kusikilizwa
Juni 12, 2008: Mwisho wa awamu ya kwanza ya sehemu ya kwanza
Septemba Mosi:Awamu ya pili (sehemu ya kwanza)
Septemba 2, 2008: Zombe, Koplo Lema wazozana
Februari 3, 2009: Koplo Lema ngonjwa
Februari 10: Zombe aanza kujitetea
Machi 2, 2009: Koplo Lema alazwa. Hali yake yabadilika
Aprili 3, 2009:Koplo Lema afariki saa 10:00 za alfajiri hospitali ya Ocean Road.
Aprili 21, 2009: Wakili wa Zombe, Moses Maira afariki akiwa Marekani
Mei 6, 2009: Mahakama yafunga rasmi ushahidi wa utetezi.
Juni 26, 2009: Majumuisho / maoni ya Wazee wa Baraza
Agosti 17. Hukumu.
*Mtu anayesadikiwa kuwa alitekeleza mauaji kwa kuwapiga risasi wafanyabiashara hao, Saad Alawi hakupatikana tangu kuanza kwa mkasa huo. |