MwanzoContactsEmail
Home Uchambuzi Maoni ya Mhariri Kwa upotoshaji huu, Ismail Jussa aombe radhi
BOOKMARK THIS PAGE
Kwa upotoshaji huu, Ismail Jussa aombe radhi  Send to a friend
Wednesday, 25 January 2012 20:53

LEO tumechapisha habari zinazomnukuu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka akishangazwa na kauli iliyotolewa katika Baraza la Wawakilishi na Mwakilishi wa Mji Mkongwe kwa tiketi ya CUF, Ismail Jussa kwamba andiko lililowakilishwa katika Umoja wa Mataifa (UN) na waziri huyo kuomba eneo la ziada nje ya maili 200 za Ukanda wa Kiuchumi Baharini (EEZ) halikufanywa kwa niaba ya Serikali ya Muungano kwa madai kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) haikushirikishwa.
   
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Waziri Tibaijuka alisema andiko hilo liliwasilishwa Januari 18 mwaka huu kama ombi la Serikali ya Jamhuri ya Muungano na kuongeza kuwa, SMZ ilishirikishwa kikamilifu tangu mchakato wa kuandaa mradi huo ulipoanza mwaka 2007.
   
Waziri alitoa kauli hiyo baada ya mwakilishi huyo kuwasilisha hoja binafsi katika Baraza la Wawakilishi mwanzoni mwa wiki, akilitaka Baraza kutolitambua andiko hilo lililowasilishwa UN na  kuliomba liiagize SMZ  kutojihusisha na mpango huo kwa namna yoyote kwa madai kwamba ni mpango wa kuhujumu eneo la bahari la Zanzibar. Mwakilishi huyo alikwenda mbele zaidi na kumtaka Waziri wa Ardhi, Ali Juma Shamhuna ajiuzulu, vinginevyo awajibishwe na Rais, huku akiungwa mkono na wajumbe waliosimama kuchangia hoja hiyo.
   
Tunampongeza Waziri Tibaijuka kwa uamuzi wake wa kukutana na waandishi wa habari jana na kuchukua muda mrefu kutoa ufafanuzi wa suala hilo ambalo tunadhani lingeweza kusababisha msuguano usiokuwa wa lazima kati ya pande mbili hizi za Muungano wetu. Tunasema hivyo kwa sababu tuhuma alizotoa mwakilishi huyo ni nzito mno pengine kuliko yeye anavyofahamu. Ndiyo maana tuhuma kama hizo zinapotolewa, serikali makini popote duniani hulazimika kuzijibu kwa ufasaha pasipo kuzibeza au kutoa majibu ya mkato kwa nia ya kuzificha chini ya zulia.
   
Hivyo ndivyo Waziri Tibaijuka alivyofanya na tunakubaliana naye kabisa aliposema alilazimika kutoa ufafanuzi wa kina kwa sababu pande hizo mbili za Muungano hazipaswi kugombea fito wakati nyumba inayojengwa ni ya wote. Moja ya sababu zinazotufanya turidhishwe na ufafanuzi wake ni pale alipotoa ushahidi wa namna Zanzibar ilivyohusishwa kikamilifu kupitia SMZ  katika ngazi zote tangu 2007, kiasi cha kuibua mashaka kama kweli mwakilishi huyo wa Mji Mkongwe alipeleka hoja hiyo barazani kwa nia njema au alidhamiria kuwachafua viongozi wa pande hizo mbili za Muungano kwa kupeleka hoja iliyojengwa kwa misingi ya maneno ya mitaani?  
   
Ufafanuzi wa Waziri Tibaijuka umetufumbua macho na sasa tumeelewa kwamba mchakato huo mkubwa na muhimu uliendeshwa na kamati mbalimbali zilizoundwa tangu mwaka 2007, ikiwamo kamati ya makatibu wakuu iliyoongozwa na Katibu Mkuu katika Wizara ya Maji, Nishati, Ujenzi na Makazi Zanzibar, Mwalimu Mwalimu na kwamba aliyekuwa Mkurugenzi wa Upimaji Ramani, Haji Adam Haji ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi. Sasa tumejua pia kwamba Pandu Makame kutoka katika Ofisi ya Makamu wa Rais ndiye aliyeteuliwa kuwa mwenyekiti mwenza wa Kamati ya Utekelezaji.
   
Tumefarijika kusikia kutoka kwa waziri huyo kuwa, zoezi la  kupima alama za sehemu ya bahari inayoombwa lililofanyika Januari mwaka jana, masheha wa Kiuyu, Maziwa Ng’ombe, Kojani na Vitongoji walioko katika Kisiwa cha Pemba walishirikishwa, huku wenzao wa Makunduchi katika kisiwa cha Unguja pia wakishirikishwa. Hata wakati wa kuwakilisha andiko hilo huko UN ujumbe wa nchi yetu uliwahusisha viongozi wa pande mbili za Muungano, akiwamo Mkurugenzi wa Sera na Mipango,  Ayoub Mohamed Mahamoud.
   
Sisi wa Mwananchi tunajivunia rekodi yetu ya muda mrefu ya kutetea haki za wananchi wa Zanzibar  pale tunapoona zinakiukwa. Lakini tumefadhaishwa na tuhuma hizo zilizotolewa dhidi ya SMZ na Serikali ya Muungano na mwakilishi huyo wa Mji Mkongwe. Tunamshauri apate ujasiri  na kuomba radhi  kwa Baraza la Wawakilishi, SMZ na Serikali ya Muungano kwa upotoshaji mkubwa alioufanya.
      
     

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #29 2012-02-03 11:22
huyu Jussa ni baradhuli la Kima[NENO BAYA]chi hana lolote kasoma sheria na mkimbizi aliyekua Uk hafai kuwa kiongozi katika taifa hili
Quote
 
 
0 #28 2012-01-31 02:21
Movie yetu ndio inaanzia hapo
Quote
 
 
0 #27 2012-01-30 08:11
JUSSA ANATUPA IMANI YA KWAMBA CHAMA CHA CUF NI KWA AJILI YA WANZIBAR TU. HUKU BARA KINAZUGA TU ILI KUKAMILISHA UWEPO WAKE KISHERIA. HAYO TULISHAYAONA SIKU NYINGI. NDO MAANA HUKU BARA SISI VIJANA HATUNA DILI NA CUF MAANA NI CHAMA CHA KIMWINYI HICHO.
Quote
 
 
+1 #26 2012-01-30 00:47
Haya sasa nendeni kwenye Baraza la Wawakilishi mkaombe nyinyi radhi kwa kimbelembele Chenu . Toka lini mkawa na uchungu na Zanzibar nyinyi na Jussa amuombe radhi nani kwa ukweli uliopo. Nyie Mwananchi ni wanafiki sana hasa kwa mambo ya Wazanzibari na leo mnaadhirika. Andikeni basi habari ya nyie kuitwa Barazani kujieleza!
Quote
 
 
-2 #25 2012-01-27 14:58
Mimi mtanganyika ukweli lazima uzungumzwe 2acheni porojo nikweli viongozi we2 wananjaa sana na wanapenda kuwalalia wazenji 2acheni ukiritimba muungano aunafaida bali ni hasara kwa wazanzibar kumbukeni karume alipo waambia raiya wake wakati wakiungana muungano ni kama koti 2kisikia joto 2nalivua sasa wanasikia joto mbona a2wapi nafasi 2mezidi kuchakachua mungu vunja nguvu za madhalimu.
Quote
 
 
+1 #24 2012-01-27 14:37
Hili gazeti ni zuri lakini baadhi ya waandishi humu wanaandika habari kwa ajili ya faida zao au mitazamo yao binafsi kwa mfano huyu alieandika habari hii inaonekana hakutaka kuandika habari za baraza la wawakilishi lakini kumbe aliskia na AKANYAMAZA KIMYA.

HALAFU NI LINI MUTATURUHUSU NA SISI KUTOKA ZNZ KUJA KUPIMA MAENEO YA TANZANITE NA LAMASI HUKO BARA?....MUSIJALI TUTAWASHIRIKISH A WATU 2 MPAKA 3, WAJUMBE WA NYUMBA 10.!!!!

Mh. Tibaijuka amepuuza azimio la BLW lilionesha mipaka ya ZNZ na na kuondosha mafuta katika mambo ya muungano. Hii inoanesha dhahiri ni jinsi gani serikali ya muungano haijali kuwepo kwa serikali ya ZNZ. na maamuzii yake.

Ikizinga[NENO BAYA] kua UCHUMI SI SULA LA MUUNGANO!!!!
Tibaijuka unataka kukuza uchumi upi?!!!
Quote
 
 
+1 #23 2012-01-27 14:08
Tanganyika haina cha kupoteza muungano ukivunjika... Wanzibari walioko Tanganyika itabidi warudi kwao...na wachache watanganyika walioko Zanzibar warudi kwao! Zanzibar wawakaribishe waarabu na misaada yao... Watanganyika wabaki na mali zao!! Kila mmoja alinde mpaka wake.. Askari wote waliotoka bara walioko Zanzibar warudi Zanzibar ianzishe jeshi lake na kila kitu chake waisi kivyao!!

Ikiwa hivi...nani ataumia!???
Quote
 
 
-3 #22 2012-01-27 11:35
Huyu Muhariri alikuwa kalewa chakari alipoandika huu utumbo nani kakwambia kama bahari ya Pemba ni ya Tanganyika acha u[NENO BAYA] wako Mwananchi, Waznzbari hawana shida ya Muungano wala katiba hamna haya Mbuzi nyinyi.
Quote
 
 
0 #21 2012-01-27 11:22
Hata Tibaijuka atoe ushahidi Wazanzibari maswala ya bahari kuu watayashughulik ia wenyewe na sio Tibaijuka au SMT.

Na kwa hilo Watanganyika hamtowahi kutuzunguka.

Jussa Hongera sana.
Quote
 
 
+1 #20 2012-01-27 11:14
Quoting mzenj halisi:
Jussa yuko sahihi na yule jamaa kipaji.
reasons: kwanza balozi idd kasema hana taarifa. 2) shamhuna kasema hajalitaarifu baraza la mapinduzi na baraza la mawaziri wala brz la wawakilishi.
4) NYINYI WATANGANYIKA MAFUTA HAYAWAHUSU SIO YENU NA HIYO TAMAA YENU. NA KWA HALI INAVYOKWENDA TUTAUVUNJA MUUNGANO. SASA TUMESHTUKA NA UADUI WENU HUO. KILA MTU KWAO KWA NINI MUNATUNG'ANG'ANIA ZANZIBAR?

NA NYINYI MWANANCHI ACHENI UNAFIKI KWANI PEMBA NI SEHEMU YENU? SI MULIUUWA WATU KIBAO PEMBA LEO WANAMAFUTA YAO YANAWATOA ROHO. ACHENI ULAFI HUO NDIO MAANA HATUUTAKI MUUNGANO BORA TUUNGANE NA KENYA KULIKO NYINYI KWANZA HATULINGANI NA MILA,UTAMADUNI, DINI NA HATA TABIA.

TAFUTENI WATU MUUNGANE SISI HATUWAPENDI, KAMA HAMUJUI SISI TUNAWACHUKUA KWELI KWELI

Kuna watu wengine ni ma-p-unguani kweli.Hivi unadhani Watanganyika wanafadika na huu muungano?wazanzibari ndo tumukuwa tukiwabeba kweli.Mpaka bili za umeme tunawalipia.Muungano ukivunjika itakuwa poa tu manake nadhani wapemba wote wataondoka Kariakoo.iNFACT HATA SS HATUWAPENDI HATA KIDOGO.TUMECHOKA KUBEBA WATU WASIO NA SHUKURANI.
Quote
 
 
-1 #19 2012-01-27 11:09
Ivi nyinyi MWANANCHI muna nia ya kweli au ajenda maalumu..? mulikuwa wapi Jusa alipowasilisha huo munaita uchochezi...nyoote mulinyamaza kimyaaa hadi tukaulizana..leo haraka Kumbe mlisikia eeh... sasa hii ni Zenji mpya...na tunasema hivi... When the hunted learns how to hunt, the hunting game is no more... na nawakumbusha ile sasa ni sauti ya Baraza la wawakilishi ambalo ni wananchi na hatuna mpango wa kumuomba mtu Radhi na hatuhitaji kuombwa.. Tunataka tu Haki iitwe Haki...Tuheshimiane udugu uendele... I repeat saying...When the hunted learns how to hunt, the hunting game is no more.!!!
Quote
 
 
-1 #18 2012-01-27 10:52
Upotoshaji huu jee?
Hivi ndio Tanzania mbili zilivyotambulis hwa. Ya kwanza ni January 2007 kwenye mambo ya mazingira na ya Pili ni January 2012 Kulaghai kupata upenu wa Zanzibar na mafuta. Ulghai wa hali ya juu huu.

I – Ya mazingira - January 2007
-----------
1. 0 INTRODUCTION & SETTING
1.1. Country Background
The United Republic of Tanzania is the largest country in the East Africa. It is located between 1 degrees
South and 12 degrees South latitude and 30 degrees East and 40 degrees east. It is constituted by
Mainland Tanzania and Tanzania Zanzibar. It is a vast country with a total area of 945,087 Sq. km
comprised of land area of 883,749 sq. km (881,289sq.km mainland and 2,460sq.km Zanzibar), plus
59,050 sq. km inland water bodies (URT, 2002a). It shares borders with eight countries. Its neighbours
include Kenya and Uganda in the North, Rwanda, Burundi and Democratic Republic of Congo in the
West, Zambia and Malawi in the South West and Mozambique in the South. [Figure 1`- Political Map of
Tanzania] Mainland Tanzania borders the main water bodies of Africa. To the east is the Indian Ocean, to
the north Lake Victoria, to the west Lake Tanganyika and to the south-west Lake Nyasa. Mainland
Tanzania also has the highest point in Africa. The snow caped Mount Kilimanjaro is 5,950 metres high.
Based on the 2002 Population and Housing Census, the country was reported to have about 34,569, 232
people: 33,584,607 from mainland Tanzania and 984,625 from Zanzibar with an annual average
intercensal growth rate (1988 – 2002) of 2.9 (URT, 2002b). By 2005 the country has about 36.2 million
people (17.7 million people were males and 18.5 million people were females).
--------------------------------------------

II – Ya Mafuta - January 2012.
==========================
2. 1.2 Tanzania is an independent, sovereign, coastal State located in the Eastern Africa region. It is bound between latitudes 1° 00’ and 11° 45’ south of the Equator and longitudes 29° 15’ and 41° 00’ east of the Greenwich meridian. Tanzania is bordered by the Republics of Kenya and Uganda to the north, Rwanda and Burundi to the northwest, Democratic Republic of Congo to the west, Republic of Zambia to the southwest, Republic of Malawi and the Republic of Mozambique to the south. Tanzania also shares the waters of the Indian Ocean with the Republics of the Seychelles and Comoros to the east and southeast, respectively.
1.3 Tanzania has an estimated population of 44,485,0002 and covers a total area of 948,740 square kilometers with land covering approximately 889,460 square kilometers. The coastline of Tanzania extends approximately 1,400 km in a north-south direction from the Tanzania-Kenya border to the Tanzania-Mozambique border to the south.

Jee unadhani haya yalifanyika kimakosa?

Source UN.
Quote
 
 
0 #17 2012-01-27 10:25
But all this still does not cover the substantive issue involved. It is well known that Foreign Affairs is a Union matter, and therefore any dealings with the UN has to involve the Minister of Foreign Affairs, even if the exact issue involves only one side of our Union. There are plenty of cases when this has been done about issues concerning non-Union matters of Mainland Tanzania. Therefore, it is not a favour to Zanzibar that once in a while the Ministry of Foreign Affairs has to take up the case when Zanzibar’s interests are concerned – it is our right, iof we are part of the Union. The same applies to the defence of Tanzania’s territorial boundaries, which include the now extended boundaries in the Indian Ocean – that is its responsibility.courtesy ofhttp://zanzinet.net/mailman/listinfo/zanzinet_zanzin et.net
Quote
 
 
+1 #16 2012-01-27 10:22
The controversy about the extension of the sea boundary has come at the right time when Zanzibaris have shown that they will no longer be hijacked when their vital national interest are at stake, regardless of party affiliation. It was rather disingenuous for Prof Tubaijuka to try to introduce party divisions when she claimed that CUF was claiming that Zanzibar was not consulted. If she heard the debate in the House of Representatives , it was almost unanimous, and prominent CCM backbenchers made a point of saying that this was not the question of CUF but of the whole of Zanzibar. She should not try to divide Zanzibaris again. We have suffered enough from such tactics.Prof Tibaijuka may be right that some people even in the Zanzibar Government may have been aware of this project, but the Minister of Lands in Zanzibar, Mr Shamhuna himself said in the House of Representatives that he know about it, but the Zanzibar Government did not know it officially. The Executive Summary of Tanzania’s submission to the UN has 2 long lists of institutions and people who were involved in this project, but mentions only Shamhuna’s Ministry of Lands out of 9 institutions, and only one State Attorney from Zanzibar out of 8 members of the Technical Core Group. Now Professor Tubaijuka mentions a few more names of Zanzibari ‘representative ’, including my friend and former student Zakia Meghji, but if my memory serves me right, she used to be an MP for Moshi, and has never pretended to be representing Zanzibar except as a person who was born in Zanzibar. This is definitely a case of desperation in looking for Zanzibari faces.But all this still does not cover the substantive issue involved. It is well known that Foreign Affairs is a Union matter, and therefore any dealings with the UN has to involve the Minister of Foreign Affairs, even if the exact issue involves only one side of our Union. There are plenty of cases when this has been done about issues concerning non-Union matters of Mainland Tanzania. Therefore, it is not a favour to Zanzibar that once in a while the Ministry of Foreign Affairs has to take up the case when Zanzibar’s interests are concerned – it is our right, iof we are part of the Union. The same applies to the defence of Tanzania’s territorial boundaries, which include the now extended boundaries in the Indian Ocean – that is its responsibility.
Quote
 
 
0 #15 2012-01-27 01:52
jusa ni mtu mdogo sana kwahiyo asitake kutuvurugia amani yetu. embu WATANZANIA kwa umoja wetu na kwa mapenzi ya nchi yetu tum[NENO BAYA]e mana UKWELI ushabainika.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner