MwanzoContactsEmail
Home Uchambuzi Barua kwa Mhariri Tumeendekeza siasa,kusahau uchumi hakika tutakwama
BOOKMARK THIS PAGE
Tumeendekeza siasa,kusahau uchumi hakika tutakwama  Send to a friend
Wednesday, 11 January 2012 09:15

Mhariri
KWA muda mrefu sasa siasa katika nchi yetu na pengine chache zinazoendelea ndiyo iliyogeuzwa mtaji na kete ya maisha.
Matokeo yake wajanja wachache wameigeuza siasa kuwa taaluma muhimu na kuwekeza ndani yake nguvu, akili na utashi wao wote.
Sasa ni dhahiri, siasa ni taaluma isiyo rasmi yenye nguvu mno na ambayo inaelekea kuwa na nguvu hata zaidi ya nyinginezo ikiwamo uchumi.

Ipo mifano mingi ya jinsi ambavyo siasa ndizo zinazojadiliwa zaidi kupitia mijadala, mihadhara (siyo ya kidini), makongamano na kadhalika au wakati mwingine wasomi waliobobea kuacha taaluma zao zikiwamo udaktari, ualimu na kuzama katika siasa.
Unaweza kujiuliza wanafuata nini huko? Ni kwamba wanaona siasa ambazo zinawafikisha bungeni au katika udiwani kama njia ya mkato ya kujipatia maisha mazuri mno.

Kwa bahati mbaya, siasa imeachiwa kutawala mambo mengi yakiwamo uchumi, kiasi kwamba ni ndara kusikia wataalam wa uchumi wakiwa wameandaa kongamano la kitaifa la kuangalia namna ya kuisaidia nchi yetu kuondonana na matatizo kama ya kushuka kwa thamani ya shilingi yetu, sababu za kuzidi kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali ambazo nyingine ni muhimu katika maisha ya kila siku.
Badala yake, watu wanasubiri makongamano katika kumbi za hoteli kubwa kubwa zilizoko Dar es Salaam au miji mingine kwa lengo la kujadili katiba mpya.

Binafsi, sipingani na hao wanaopigania kupatikana kwa katiba mpya, ila najiuliza, vipi uchumi wetu ambao unadumaa na kupooza kila uchao, mbona hakuna mahali ambao wataalam wake na wadau wengine wanakutana na kuangalia nini kifanyike, kuweka mikakati ya kusogea mbele?

Hata wakati mwingine unasikia makongamano kama ya kujadili hali ya siasa katika Tanzania na kisha yanapitishwa maazimio, lakini sikumbuki tunaazimia nini katika uchumi, biashara au afya!
Kwa mtazamo wangu, naamini kwamba hali hii itatufanya kama nchi tuzidi kuwa duni, maskini zaidi kama suala la uchumi linaachwa kama yatima, macho na masikio yetu yanaelekezwa zaidi kwenye mijadala ya siasa ikiwamo ya watu au wanachama kufukuzana uanachama kama ambavyo imetopkea kwa vyama  vya NCCR- Mageuzi na CUF hivi karibuni.

Kama mwanajamii katika Tanzania, ninaamini kuwa hata Wizara ya Fedha na  Uchumi, wataalam wake wanatakiwa kushirikiana na wengine kama wa Kilimo, Ushirika, Biashara na kuangalia jinsi ambavyo tutapiga hatua na kuiondoa nchi yetu katika janga hilo la umaskini wa kupindukia.
Isidori Ndyamukama,
Kijichi-DSM


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner