MwanzoContactsEmail
Home Uchambuzi Barua kwa Mhariri ARVS zinazotumika Tanzania zipatiwe mbadala
BOOKMARK THIS PAGE
ARVS zinazotumika Tanzania zipatiwe mbadala  Send to a friend
Friday, 13 January 2012 10:12

Mhariri

NASHUKURU kwa kupata nafasi katika gazeti lako  nilipendalo ili niweze kusema  machache niliyo nayo kuhusu ugonjwa  hatari wa Ukimwi katika Tanzania na dawa za kurefusha maisha, ARVs.

Nafahamu kuwa ugonjwa huu haujaingia Tanzania pekee, bali ni Afrika na duniani kote.

Lakini wanasema hapa nchini kwetu, ugonjwa huu umefanya mashambulizi na bado unaendelea na mashambulizi hayo.

Pamoja na kupatikana kwa dawa hizo za kupunguza makali ya ugonjwa huu, ARVs, lakini bado changamoto zimekuwa nyingi.

Kwa mfano, Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) lilitangaza kuwa, dawa hizo hazina usalama kwa asilimia 100.

Sasa kama siyo salama kwa kiasi hiki mbona Serikali yetu, hasa Wizara ya Afya ipo kimya wakati Watanzania wengi wanazitumia?

Tunaiomba Serikali itafute suluhisho, na si suluhisho la ARVs pekee, bali na tiba kamili ya kutibu ugonjwa huu.

Tunataka tiba na si kupunguza makali kwani mpaka hivi sasa watu wameshapoteza  fedha nyingi kwenda Loliondo kwa Mchungaji Ambilike Mwasapila na tiba kadha wa kadha lakini hawajapata suluhisho.

Si hivyo tu, hizi kampeni za matumizi ya mipira ya kiume nazo zinazidi kuongeza tabia hatarishi kwani ‘condoms’ nazo si kinga ya kuaminika sana.

Serikali itusaidie kutafuta tiba ya kuangamiza ugonjwa huu, kwani bila kufanya hivyo taifa lote litamalizika.

Fatuma Namwadilanga,
Masasi-MTWARA. 


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner