MwanzoContactsEmail
Home Uchambuzi Barua kwa Mhariri Walimu watanyanyasika mpaka lini?
BOOKMARK THIS PAGE
Walimu watanyanyasika mpaka lini?  Send to a friend
Tuesday, 17 January 2012 09:07

HIVI  kwa nini Serikali hasa hii ya awamu ya nne itatunyanyasa walimu?
Hii ndiyo Serikali ambayo  viongozi wake wengi wanajilimbikizia mali. Wao na familia zao wanaishi kama wako peponi hali wananchi wa kawaida kama walimu tukiteseka kwa kiasi kikubwa.
Viongozi wetu kuanzia ngazi za chini  hawaelewi matatizo yetu! Kama haitoshi, Serikali inatoa nyaraka za kuwadidimiza, kuwanyanyapaa  kuwaondolea utu wao na kuwadharau walimu tena wazi wazi.

Mfano ni  hivi sasa  hata mwalimu akisoma, ngazi yake ya mshahara inabaki palepale! Ewe Waziri wa Utumishi wa Umma na Katibu Mkuu wako. Enyi mawaziri husika na makatibu wakuu, mngekuwa walimu sijui kama mngefurahia mambo haya.

Najua aliyeshiba hamjui mwenye njaa, lakini msifanye waziwazi kuionyesha jamii kwamba kazi ya ualimu ni ya kukimbilia tu kama maisha yameshindikana.

Naomba muithamini kama kazi nyingine. Maofisa elimu hawazioni  nyaraka hizi kama  zinawanyanyasa walimu, kwa kuwa wao na familia zao wana maisha mazuri.

Wanabaki kusema  walimu fanyeni kazi, lakini hawaangalii upande wa pili kwamba walimu wanaishi katika dimbwi la umaskini, hawajui kesho yao itakuwaje. Maofisa hawa wanaangalia matumbo yao na familia zao tu.

Namkumbuka Ofisa Elimu  mkoa wa katika mkoa mmoja uliopo  nyanda za juu kusini, anapoongea na walimu huwa anawachukulia kama watoto wadogo au watoto zake na kuwadharau, kuwadhalilisha hata wale wenye  umri kama wa baba yake.

Kweli haipendezi na  sio sahihi hata kidogo. Nawaomba wasimame kuwatetea walimu na sio kuwakandamiza na kuwadidimiza kila kukicha.

Mwalimu Baraka Mushi

Mbeya

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #2 2012-01-23 13:07
I would like to thanks a ton for the work you've put in writing this web site. I am hoping the same high-grade webpage post from you in the upcoming also. The fact is your original writing abilities has inspired me to get my own site now. Actually the blogging is spreading its wings fast. Your write up is the best example of it.
Quote
 
 
+2 #1 2012-01-17 17:01
Walimu lazima wanyanyasike kwasababu kuu moja ambayo ni kutojiami na kutoamini taaluma yao. kwamfano,
-walim hawajosomea mambo ya mwenge{uhuru torch} lakin ndio wa kwanza kupokea na kupika chakula cha kwenye mwenge
-wao ndio vinara wa kuacha kufanya kazi walizosomea (kufundisha) na kupokea wabunge, mawaziri na viongozi wengine wa kitaifa
-walimu hawana sauti moja [kuna matabaka miongoni mwa wale wenye vyeti, stashahada na wale wenyeshahada.
wangekuwa na sauti moja wangefanya maamuzi magum walipoitwa makanjanja na mbayuwayu.
lazima wanyanyasike.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner