MwanzoContactsEmail
Home Uchambuzi Barua kwa Mhariri Leseni mpya ni kukusanya mapato, kulinda ajira za madereva au kupunguza ajali?
BOOKMARK THIS PAGE
Leseni mpya ni kukusanya mapato, kulinda ajira za madereva au kupunguza ajali?  Send to a friend
Thursday, 19 January 2012 10:37

Na Zakie Chatanda
SWALI langu kubwa, je hizi leseni mpya za madereva ni kwa ajili ya kukusanya mapato ya serikali, kulinda ajira za madereva au kukabiliana na ajali?
Nafikiri siyo mimi peke yangu  ambaye najiuliza swali hili. Kuna watanzania wengi hasa madereva ambao ninawawakilisha.
Hatua ya kubadilisha leseni za udereva ilichukuliwa na serikali ili kukabiliana na ongezeko la idadi kubwa ya ajali za barabarani ambazo zimesababisha   vifo kadhaa na majeruhi .

Sababu kubwa ya ajali ilitajwa kuwa leseni nyingi hasa zile za daraja la C ama zilitolewa kwa wasiostahili au wengi walizipata kwa njia za ujanja ujanja. Hatua hiyo ingesaidia kubaini leseni bandia na zilizotolewa bila ya wahusika kufanyiwa bila kupitia mafunzo maalum na kuruhusu kuanzishwa kwa mfumo wa kisasa wa kutunza kumbukumbu za leseni na madereva vizuri.

Suala la pili ilikuwa ni kuboresha leseni yaani kuondokana na mfumo wa sasa ambao ni wa kizamani na kuzibadilisha kuwa katika mtindo wa kisasa yaani za kielektronika. Mfumo utakuwa rahisi kujua taarifa za kila ambaye ana leseni ya kuendesha gari nchini.

Suala la tatu ni kusaidia kutunza kumbukumbu za madereva na leseni zao baada ya kubadilisha leseni kwani asilimia kubwa leseni zilizotolewa zamani takwimu zake zilikuwa zinahifadhiwa kwenye vitabu hivyo ilikuwa ni vigumu hata kujua idadi ya madereva nchini.

Hatuna budi kuipongeza serikali, Mamlaka ya Mapato (TRA) pamoja na Jeshi la Polisi kwa hatua hii nzuri kwani mbali na kupunguza au kutokomeza ajali nchini pia leseni za madereva wetu zitakuwa zina  mvuto, muundo wa kisasa na vile vile kumbukumbu zao zitakuzwa zinahifadhiwa kisasa zaidi.

Dosari la hii kazi kubwa inakuja pale tu, serikali inapotaka kugeuza shughuli hii kwa ajili ya kukusanya mapato zaidi na hivyo kufifisha madhumuni yake tuliyoambiwa wakati wa kutangazwa kwa nia ya kuanzisha zoezi hilo.
Madereva wa daraja la ‘C’ wanaambiwa kurejea madarasani ili kupata vyeti kabla ya kubadilishiwa leseni.

Ada kwa ajili ya mafunzo hayo ambayo yanachukua siku 10 tu inafikia Sh200,000. Kiwango hicho ni kikubwa mno na gharama zake haziwiani na mafunzo mafunzo anayohitaji dereva mzoefu wala hata na vipato vya madereva wengi nchini. Serikali inapaswa kukumbuka mara kadhaa madereva hao wametishia kugoma kutokana na ujira mdogo kutoka kwa wajiri wao.

Ninaamini kuwa madereva wengi watakosa fursa ya kubadilisha leseni kwa kutokuwa na fedha. Hii itawafanya wengi kusaka vyeti kwa njia ya mkato ili waweze kubadilisha leseni zao au wengine watabaki majumbani na hivyo kuongeza jeshi la wasio na kazi nchini.
Kibaya zaidi gharama hiyo ya Sh200, 000 haijumuishi gharama ya leseni ambayo ni Sh40, 000. Kwa hiyo anataka kubadilisha leseni anapaswa kuwa na Sh240, 000. Tunaikumbusha serikali kuwa madereva wengi mishahara yao haizidi Sh300, 000.

Jambo jingine ambalo ninaliona kuwa ni dosari kubwa katika zoezi zima la kubadilisha leseni ni kitendo cha kuwataka kufanya hivyo hata kama kama zile walizonazo hazijamalizika muda wake. Ni leseni zilizotolewa na mamlaka hiyo hiyo. Hii maana yake ni nini? Ningeelewa kama zoezi hilo lingewagusa wale ambao leseni zao zimekwisha muda.

Katika hili serikali imekosea ilipaswa kuheshimu ukomo wa leseni ilizozitoa ili dereva akitaka kuongeza muda ‘renew’ ndiyo apewe leseni mpya badala ya ile ya zamani hii itaondoa machungu kwa baadhi ya madereva kwa sababu wengi wao leseni zao wamebadilisha mwaka jana na inatakiwa wakae nazo miaka mitatu kabla ya miaka hiyo haijaisha au hata miezi sita wanaambiwa kuzibadilisha tena kwa gharama kubwa zaidi na baada ya mafunzo maalum.

Madereva wengi wameshindwa kubadilisha leseni zao katika muda uliopangwa  wa Desemba 31, 2011. Jambo hilo lisababisha tafrani na taharuki pale mabasi mengi yaliposhindwa kufanya safari kwa kuwa madereva wengi hawakuwa na leseni mpya. Januari 6, 2012 serikali ililazmika kuongeza muda bila kutaja ukomo wake.
Nilikuwa nashauri hivi, badala ya serikali kujikanganya namna hii ni heri ikaweka suala hili wazi kuwa madereva wenye leseni za zamani ambazo hazijaisha muda wake waendelee kuzitumia lakini zikiisha muda wakati wa kuongeza muda basi wahakikishe wanapata leseni mpya.

Kuliko hivi sasa serikali kuwakimbiza kimbiza madereva kubadilisha leseni kitu ambacho mimi binafsi naona ni kibaya kwani kinaongeza mianya ya rushwa sehemu za kubadilishia leseni pamoja na vyuoni kwani madereva wengi watanunua vyeti badala ya kupata elimu husika.

Hili la kuwataka madereva kubadilishe leseni zao huku serikali ikijua kuwa bado hazijaisha muda siyo utawala bora na wengi tunaitafsiri hatua hii kuwa ni mkakati wa serikali wa kukusanya pesa kutoka kwa watanzania ambao tayari wanakabiliwa na maisha magumu.

Tunadhani serikali inapaswa kutafuta njia nyingienya kutafuta pesa kwa ajili ya kuendesha nchi pasi na kuwatia jakamoyo wananchi. Zoezi hili la kubadilisha leseni ni kero. Ni zoezi ambalo halitapunguza ajali wala kuboresha ajira za madereva nchini Tanzania.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #4 2012-01-24 10:30
Inawezekana leseni mpya ni mradi wa mtu fulani kama ilivyo miradi mingine nchini. Lakini ninaamini leseni mpya kama zitaendelea kutumika kwa namna ya mfumo wa kidigitali kama zinavyotolewa; basi ajali za barabarani zitapungua. Matrafiki wanaweza wakauza leseni lakini hazitakuwa na file, hivyo mtoa rushwa hiyo atakuwa kapata hasara mwenyewe. Kwahiyo mimi nashauri kwamba mfumo wa utoaji wa leseni hizi haswa daraja C ukiendelea kama ulivyoanza mwanzoni; yani usipochakachuli wa; basi ajali zitapungua sana na baadaye kuisha.
Quote
 
 
0 #3 2012-01-23 16:16
Hapa kwetu tunachanganya Mambo na vitu; Siasa katika taaluma.
Tunao majirani zetu kama Kongo,Luanda,Ke nya,Uganda. Wanafuata Kanuni na Sheria vema sana, tofauti na Tanzania/Tanganyika. Hapa ni mchanganyiko wa vitisho na Uroho wa Rushwa tupu kuharibu hata baadhi ya makusudio mazuri yanaingia pabaya kila siku.pia tunaishi kwa MAtukio/Ajari hapo kila kiongozi hujaribu kutoa matamko makali.Jeshi la polisi livunjwe na kuundwa upya kama taasisi.
Quote
 
 
+1 #2 2012-01-22 22:23
Serikali Inabadilisha Lisensi,jee Itawadilisha hao mapolisi wanotoa hizo liseni kwa kupokea rushwa??
Quote
 
 
0 #1 2012-01-20 10:51
Asante kwa Makala,ila sidhani kama jambo hili halifahamiki kwa wahusika kwani nao ndipo wanapatia,huwez i badili gamba ukaamini umerekebisha mfumo mzima wa mwili,unajua kuna mambo ambayo lazima serikali na watunga sera wake wajaribu kupitia,si rahisi hata kidogo kutuambia kwamba tukibadili leseni tutakuwa tumekabili tatizo la ajali,hata kidogo mimi nadhani lazima watu waumize vichwa hapa tulikuwa na vyuo vilivyopaswa kuendesha elimu hii si tu kwa waajiriwa wa serikalini au madereva wa mawaziri ila hata kwa hawa wanao pewa dhamana ya magari ya abiria,lakini wapi idadi ya wahitimu ni ndogo kuli mahitaji, sasa unategemea nini hapa hivi bomu tumelitengeneza tunaliogopa wenyewe,kama tumeshazoezwa vya kunyonga je tutaweza kuchinja.Ajali za barabarani zina sababu nyingi na zote ni muhimu kurekebishwa,hi vi kwanini kama hatuwezi kupembua mambo tusi copy na kupest twende kenya tuangalie wanafanya vipi tuje tupest hapa kwetu.
Tulikuwa na system ambayo ingeongeza tija katika tatizo la ajali RATIBA ZA MUDA WA SAFARI lakini wapi bwana nani anajuazilipo fia,hapa ni kutafuta hela na si vinginevyo,hivi tujaribu kuulizana nani atakae kuwa anajua dereva fulani kafungiwa kuendesha magari kutokana na ajali,hivi dereva huyu akitoka dar-moshi akaenda masasi-mtwara kuna raia atakae mtambua?jibu hapana ni traffic police pekee nae tena mpaka amkamate na kosa waende kituoni ndio atakuwa na jinsi ya kumtambua,na kwa dereva kwenda kituoni wakati unajua leseni yako imeshafungiwa haitawezekana mtayamaliza na askari pembeni sasa pana nini hapo.Kama msoni alie elimika anataka maisha ya anasa ndani ya miaka yake michache ya ajira ndivyo kwa hata askari wetu je ninani atakae simamia sheria
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner