MwanzoContactsEmail
Home Uchambuzi Kolamu Bwagamoyo:Igunda kipimo sahihi cha siasa za CCM, Chadema
BOOKMARK THIS PAGE
Bwagamoyo:Igunda kipimo sahihi cha siasa za CCM, Chadema  Send to a friend
Saturday, 10 September 2011 17:07



L. W. Nzela

MATOKEO ya uchaguzi mdogo katika Jimbo Igunga yatatoa jibu sahihi ya ni siasa za chama gani zinakubalika zaidi nchini sasa hivi. Uchaguzi huu mdogo ambao kampenzi zake zimeanza wiki hii unafanyika kufuatia kujiuzulu kwa mbunge wa muda mrefu wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Rostam Aziz kufuatia shinikizo kubwa la kuhusishwa kwake na kashfa mbalimbali za kifisadi nchini na mgongano wa kisiasa ndani ya chama hicho. 

Baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana vyama vikuu vya siasa nchini CCM na Chadem viliamua kufanya siasa tofauti ambazo zimeendelea kuligawa taifa. Siasa hizi zinaenda kujaribiwa matokeo yake huko Igunda kwani siasa zenyewe zimetokana na kukuzwa kwa namna moja au nyingine na Rostam Aziz akiwa mbunge na yumkini mwanasiasa mwenye nguvu zaidi ndani ya CCN. 

Kwa wa CCM siasa zake zilijikuta zikipoteza mvuto kuliko wakati mwingine wowote wa historia yake. Siasa zake zilijengwa katika msingi wa kile tunachoweza kukiita “kuonesha mafanikio” ya CCM,  hivyo walitumia muda mrefu kuelezea na kuwafanya watu waone “mafanikio” na kuwa kwa kufanya hivyo basi wapiga kura wataona sababu ya kuendelea kuichagua CCM.

Ni katika mwelekeo wa mawazo hayo viongozi wa CCM walijikita katika kubeza wale ambao “hawaoni mazuri yaliyofanywa na CCM” na hivyo kuwafanya watu waone mazuri na wakiona mazuri wakubali kuwachagua wagombea wake. Naamini ni mkakati huu huu utatumika tena Igunga. CCM itajaribu kuonyesha mambo mbalimbali ambayo yamefanywa na Serikali hiyo, mbunge aliyejiuzulu na hata Serikali ziliopita huko Igunga. 

CCM itajihidi kuonyesha kuwa siasa za mahali (local politics) za pale Igunga zinaonesha pasipo shaka kuwa CCM inakubalika kwani imefanya mengi. Ili hoja hii ifanikiwe hata hivyo naamini itabidi iwe tofauti na hoja zilizopita ambapo wingi wa vitu vilivyofanywa na CCM ndio ulikuwa unatiliwa mkazo zaidi. Kwamba Serikali imejenga shule nyingi, kliniki nyingi, wanafunzi wengi, barabara nyingi, n.k 

Tatizo la hoja za wingi ni kuwa watu wataanza kuuliza ubora. Je, katika hivyo vitu vingi ni vipi viko bora? Je, elimu inayotolewa ni bora kiasi gani? Je, wanafunzi kwenye hizo shule nyingi wanafauli kwa kiasi gani kulinganishwa na wanafunzi wa sehemu nyingine? Haya ni maswali ambayo upinzani unaweza kabisa kuyatumia kubomoa hoja ya “mafanikio”. 

Lakini CCM haikuishia hapo. Baada ya kufanya vibaya kwenye uchaguzi uliopita kulinganisha na chaguzi zilizotangulia CCM iliamua kuanza kujichunguza na kujisafisha katika kile ambacho kinajulikana kwa umaarufu kama “kujivua gamba”. 

Jinsi jambo hilo lilivyopigiwa panda wakati wake kulifanya watu waamini kabisa kuwa ni wakati wa CCM kujisafisha na hasa pale ambapo mafisadi ndani ya chama hicho iliposemwa kuwa wamepewa siku tisini kujiuzulu nafasi zao. 

Kwa kadiri siku zilivyozidi kwenda ndivyo maana ya kujivua gamba ilipozidi kupanuliwa na kufafanuliwa zaidi na zile siku tisini zilipopita ikajulikana wazi kuwa juhudi za kujivua gamba hazikuwa rahisi tena. Hili la CCM kushindwa kujisafisha hadi kupata hisani ya Rostam kujiuzulu mwenyewe huko wenzake wakiweka ngumu kunaweza kutumiwa vizuri kabisa na upinzani kuonesha jinsi gani CCM imekuwa dhaifu na kwamba siyo ile CCM ambayo wanaigunga walikuwa wanaifahamu zamani.

Kwa upande wa Chadema siasa zake kabla ya uchaguzi mkuu zilikuwa katika kuonesha udhaifu na ubovu wa nchi chini ya CCM. Kwa kifupi Chadema ilijaribu kuonyesha kuwa kile kinachoitwa “mafanikio” kilikuwa ni “majaribio yaliyoshindwa”. 

Kwa muda mrefu walifanikiwa sana kuonesha kuwa kama CCM ingeweza kutawala vizuri zaidi na kusimamia vizuri raslimali zetu Tanzania ingekuwa zaidi ya ilipo sasa. 

Kimsingi, CDM walikataa kukubali kuwa tulipo hapa kama taifa ni matokeo ya kazi nzuri ya uongozi wa CCM. Hoja hii ilikubaliwa sana, kwani wakitumia mifano ya nyumba za tembe na matatizo ya wananchi waliweza kuwashawishi wananchi kuwa walichokipata sicho walichokistahili. Kwamba tatizo halikuwa kukosekana tu kwa shule za kata bali ubora wa shule hizo, kwamba tatizo halikuwa kukosekana tu kwa vitu bali ubora wa vitu vilivyopo.

Na walienda mbele zaidi kwamba, baadhi ya matatizo yalisababishwa na vigogo wa CCM na ni matatizo ambayo yalikuwa na matokeo ya moja kwa moja katika maisha ya Watanzania. Hivyo, walipotangaza orodha yao ya aibu ya mafisadi na walipowakomalia kina Chenge, Rostam, Mkapa, Lowassa na wengine ilikuwa ni katika kuonyesha kuwa matatizo ya Watanzania yanahusiana moja kwa moja na baadhi ya vigogo wa chama tawala. Matokeo yake Chadema ikajikuta inajizolea kura nyingi zaidi na kukubalika zaidi kuanzia vijijini na mijini. 

Na baada ya uchaguzi huo ChademaM ikaamua kuchukua siasa za migongano (confrontational politics) kuanzia kususia hotuba ya Rais Kikwete Bungeni Dodoma kwenye kikao cha kwanza cha Bunge hili na baadaye kampeni za maandamano za kufanya mashinikizo mbalimbali na kufanya watawala wakose raha kabisa. Siasa hizi za migongano na maandamano zitaenda kujaribiwa matokeo yake huko Igunga. 

Lakini siasa hizi zinaweza kutumiwa vizuri tu kinyume na CCM kwa kuonyesha kuwa siasa za migongano zina matokeo mabaya kwa jamii wakitolea mifano ya Syria na Libya na wakati huo huo kuonyesha kuwa Chadema inachochea “nchi isitawalike”. 

Kama CCM ikijipanga vizuri kuonesha madhaifu ya Chadema kama chama na kuwa kinakabiliwa na changamoto zile zile za zamani kinaweza kupunguza makali yake. 

Kwa mfano, suala la posho za vikao linaweza kutumiwa vizuri kabisa na CCM kuonesha kuwa Chadema kama chama hakina msimamo mmoja wala hakiwezi kusimama pamoja. Mgongano wa nani anapokea posho na nani anataka posho japo unaweza kutajwa ni ‘tofauti za kisiasa’ umeonesha tu kuwa kuwa siyo wote ndani ya Chadema wanaaamini kile ambacho chama kinaamini kwenye mambo ya msingi. Mgongano wao na Shibuda ni mgongano ambao unaweza kutumiwa vizuri na CCM. 

Kwa ufupi ni kuwa atakayeshinda Igunga atakuwa siyo yule aliyeimba sana au aliyekuwa na watu wengi kwenye mikutano yake bali yule aliyeweza kumfanya mwenzake akataliwe na asikubalike. Yaani, yule ambaye kwa upande wa CCM ataweza kuzileta siasa za mahali na kuzipa matumaini ya siasa za kitaifa na kwa upande wa Chadema siasa za kitaifa na kuzileta kuzipa mwanga wa siasa za mahali. 

Nani atashinda? Naamini baada ya kama wiki mbili za kampeni tutapata picha nzuri ya nani anaelekea kuvutia watu zaidi kwa hoja zake. Tutaweza kutabiri kwa uhakika zaidi wakati huo.

Niandikie: This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #9 2011-09-22 13:40
da ccm ni kiwavi jeshi msimu ukifika vinajaa msimu ukiisha vinakufa yaani wapo kimaslai hawafai hata kidogo mkapa toka ang"oke madalakani heti ndio leo hii ankuja huku aoni aibu jamani ilo ni balaa wana igunga choo cha kike tufanye mahamuzi sahihi sio ushabiki maskini tunaisha kwa vifo.njooni muone muhimbili.
Quote
 
 
0 #8 2011-09-19 10:30
Na inashangaza sana kuwa nani anayemwaga damu hadi sasa. Igunga wanachofanya nini? Najua watu hawaioni ccm inafanya nini lakini iko siku macho yao yatawafungunga na bila shaka tuko mbioni kuwaelimisha.
Madhaifu ni madhaifu tu hakuna dhambi ndogo. Kumbuka wafadhili wa cdm ni makapi ya ccm. (Mrema Arusha, Maswa, Na wahindi wanaowapa mamilioni ili mkiingia mmwape makandarasi. nani asiyewafahamu?)
Quote
 
 
0 #7 2011-09-18 06:33
Ccm ni magaidi na wezi tu wako tayari kuhakikisha wanabaki madarakani hata kwa kumwaga damu! Hebu tazama hii!
youtube.com/.../...">
Quote
 
 
0 #6 2011-09-17 13:07
Madhaifu ya chadema ni nafuu kuliko ya CCM na kama wewe ni tajiri ni vigumu kuyaona ila utaishia kutetea, maskini wa nchi hii ndo tuyaona kwa jicho la tatu
Quote
 
 
0 #5 2011-09-16 10:55
Mhariri, Angalia sasa mawazo ya watu wako (George na Sikokyi) Ni mawazo ya wahuni wa mtaani wafuta banki na wala madwa ya kulevya. Hawana mawazo ya kuisaidia nchi hii. Kama ww umepata mawazo gani ya kujenga kwa hawa watu wawili. Ndiyo WaTZ wanaotaka kujenga TZ tunaoitaka. Haki nakwambia tumekwisha. Na hawa nakwambia yawezekana ni vijana wenye kuweza kutoa mwazo constructive lakini hapo ndiyo mwisho wa mawazo yao. TUMEKWISHAAAAAA AAAAAAAAA. TZ TUAMUKE TUONE HAWA WANATUPELEKA WAPI.
Quote
 
 
0 #4 2011-09-16 10:48
Mimi ni mwanaccm. Kinachonisikiti sha zaidi cdm sasa wanaona wana haki kwa kila mtu. Kumpiga kiongozi ni kukiuka haki zake kama raia, na pia haki zake kama kiongozi. Ni lazima sasa ccm ione kuwa hawa watu hawana haki kuwapeleka hivyo. Na watambue uhalali wao popote walipo. Ni vizuri pia waone kuwa ss ni Watz na tuna haki zote nchi hii. (Fisi ni myama tunayeamini kuwa ni mwoga sana lakini kama unataka kujua ukali wake we mbananishe maali hapo utaona ukali wake) sasa ccm tuamuke, hatujaua wala hatuja fanya lolote baya ni kwa vile hatujitambui kama kuna mwenzetu aliyefanya hivyo. Tuamke sasa.
Quote
 
 
0 #3 2011-09-16 10:41
Ndg mhariri, nakubaliana nawe kwa asilia nyingi tu. Na napenda kuongeza kuwa pamoja na vyma hivi viwili kuwa na matatizo ma mafanikio hayo viongozi wanashindwa kuelewa kuwa mafanikio hayo yanaletwwa na wananchi wa kawaida kabisa. Sina shaka kuona kaburi la cdm linajengwa na udikiteta uliojengeka kwenye ngazi ya juu ya uongozi na hapo ndipo tutakapoona uongozi wa kidicteta kwa mara ya kwanza hapa tz. Angalia maamuzi ya madiwani wa arusha, matisho kwa viongozi wenzao bila kujali kuwa viongozi hao wamewekwa na wananchi. Ni mawazo ya cdm kuwa mtu anayeisifu ccm kachanganyikiwa na kuona kuwa wao wako wasafi sana. Kitu ambacho sio kweli.
Quote
 
 
-1 #2 2011-09-15 19:53
Uzuri sisi wananchi tunaelewa sasa kuwa nyie waandishi wa mwananchi mmshapokea ile rushwa ili muweze kuipamba CCM kama ulivyo jipambanua katika makala yako hapo juu, akili zenu hovyooooooooooo o kama hongo mliyopeewa
Quote
 
 
-1 #1 2011-09-14 20:02
karudie kufanya uchunguzi na ulete taarifa za kweli na zenye uhakika kuhusu haya uloyasema na si kuwa katika mlengo mmoja wa chama fulani
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner