Arsenal wenyeji wa Napoli Uefa Europa League

Klabu ya Arsenal itacheza na Napoli mechi ya robo fainali ya Uefa Europa League mchezo ambao ni baada ya droo hiyo kufanyika leo Ijumaa.

Mbali na mchezo huo, Slavia Praha watakuwa wenyeji wa Chelsea, Benfica itacheza na Eintracht wakati Villarreal watawakaribisha Valencia.

Katika mechi hizo ambazo zinachezwa nyumbani na ugenini zitapigwa siku moja ya Aprili 11 katika viwanja vinne tofauti.

Katika fainali hizo bingwa mtetezi ni Atretico Madrid ambao waliyaaga mapema mashindano hayo.