Kumekucha fainali za AFCON, bei ya tiketi za ndege yatangazwa

Muktasari:

  • Hatua hiyo Taifa Stars itacheza michezo mitatu ambapo itaanza dhidi ya Senegal ikifuatiwa na mchezo dhidi ya Kenya na kumalizia hatua hiyo kwa kucheza na Algeria

Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limetangaza gharama za tiketi za kutazama mechi za Fainali ya Africa (AFCON) inayotarajia kuanza mwezi ujao nchini Misri.

Kwenye michezo ya hatua ya makundi ambayo itahusisha timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars” tiketi za daraja la 1 USD 29,tiketi za daraja la 2 USD 18 na tiketi za daraja la 3 USD 6,

Hatua hiyo Taifa Stars itacheza michezo mitatu ambapo itaanza dhidi ya Senegal ikifuatiwa na mchezo dhidi ya Kenya na kumalizia hatua hiyo kwa kucheza na Algeria

Kwenye hatua ya robo fainali gharama ya tiketi daraja 1 USD 35 kwa daraja la 2 USD 24 na daraja la 3 USD 12

Hatua ya nusu fainali daraja la 1 USD 59,daraja la 2 USD 29 na daraja la 3 USD 18

Wakati mchezo wa mshindi wa 3  itakua USD 35 daraja la 1,USD 24 daraja la 2 na USD 12 daraja la 3.

Mchezo wa fainali daraja la 1 USD 106,daraja la 2 USD 44 na daraja la 3 USD 24.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa yeyote mwenye nia ya kununua tiketi hizo za AFCON awasiliane na TFF mapema kabla ya kufungwa kwa muda wa maombi.