Serengeti Boys, Uganda zafuta ndoto kushiriki Kombe la Dunia

Muktasari:

Kwenye Kundi A, Angola na Nigeria ndizo zimepata nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia baadaye mwaka huu.

Tanzania U-17 Serengeti Boys imepoteza michezo yote mitatu ya kundi A baada ya kufungwa mabao 4-2 dhidi ya Angola U-17 kwenye mchezo wa fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon)

Mashabiki waliofika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam waliendelea na shangwe kama kawaida licha ya timu hiyo kuonekana kupoteana kimchezo uwanjani.

Vikundi viwili, kimoja jukwaa ambalo hupenda kukaa mashabiki wa Yanga na kingine upande wale wa Simba vimekuwa mstari wa mbele katika kushangilia.

Huu ni mzuka wenyewe wa soka kwani vikundi hivyo ndiyo vimewapa mzuka zaidi mashabiki wengine wanaonekana uwanjani hapa wakiwa mmoja mmoja.

Awali, Serengeti Boys ilikuwa inahitaji ushindi wa manne zaidi mbele ya Angola. Kikosi hicho, ipo Kundi A katika mshindano ya AFCON pamoja na Nigeria, Angola na Uganda.

Mashindano  hayo ya vijana chini ya miaka 17 ya AFCON yanaendelea kutimua vumbi jijini Dar es Salaam na timu mwenyeji ni Serenngeti Boys.

Kwenye Kundi hilo Angola na Nigeria ndizo zimepata nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia baadaye mwaka huu.