Simba OUT ligi ya Mabingwa Afrika

Muktasari:

  • Simba imetolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya leo Jumamosi kuchapwa mabao 4-1 na TP Mazembe ya  DR Congo.

Huo unakuwa mwendelezo wa Simba kupoteza mechi  za ugenini kwani tangu hatua ya makundi walipoteza mechi tatu kwa mabao 5-0 dhidi ya AS Vita ya Congo na Al Ahly ya Misri na mabao 2-0 kutoka kwa JS Saoura ya Algeria hivyo katika mchezo minne ya ugenini imeruhusu mabao 16.
Katika mchezo huo wa  Robo fainali uliofanyika kwenye Uwanja wa Stade TP Mazembe Lubumbashi DR Congo Simba ilionekana kuzididwa muda mwingi wa mchezo huku safu ya ulinzi ikionyesha udhaifu mkubwa.
Licha ya Simba kuanza kufunga bao dakika ya pili kupitia kwa Emmanuel Okwi lakini haikuwasaidia kuepuka kipigo hicho kikubwa na kuendeleza rekodi yao mbovu ya kupoteza mechi za ugenini tangu hatua ya makundi ya  mashindano hayo.
Simba ndio ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya pili tu ya mchezo lililofungwa na Emmanuel Okwi ambaye alimalizia pasi safi ya Haruna Niyonzima.
Kuingia kwa bao hilo kuliwanyong'onyesha mashabiki wa TP ambao walibaki wameduaaa na kuacha kushangilia.
Dakika ya 21 Kabaso Chongo aliisawazishia TP Mazembe bao  kwa shuti la kawaida baada ya wachezaji wa Simba kujichanganya kuokoa mpira wa kona uliopigwa na Rainford Kalaba.
Meshack Elia aliipatia  TP Mazembe bao la pili dakika ya 38 baada ya mabeki wa Simba, Juuko Murshid na Zama Coulibaly kujichanganya wakati wakiokoa kabla ya  mkongwe Tresor Mputu kuipatia timu yake bao la tatu dakika ya 62 kwa shuti kali nma kufikisha mabao matano katika mashindano hayo.
 TP Mazembe hawakulizika kwani waliendelea kufanya mashabulizi mengi golini jkwa Simba na kufanikiwa kuandika bao la nne dakika ya 75 kupitia kwa
Jackson Muleka  ambaye naye amefikisha mabao matano sawa na Mputu na Clatous Chama wa Simba.