Vita ya Ufungaji Afcon usipime

Muktasari:

Kasi ya kugombea mfungaji bora katika Fainali za Afcon imezidi kushika kasi

 STRAIKA Osvaldo Pedro amegeuka kuwa mshambuliaji tishio baada ya kufunga magoli matatu katika mechi tatu za Fainali za Afcon (U17) zinazoendelea nchini.

Mshambuliaji huyo wa Angola anafukuziwa na Edmund John, Ubani Wisdom, Jabaar Ibraheem, Seidou Ismaila na Tawfik Bentayeb ambao wana magoli mawili wote.

Mshmabuliaji wa Serengeti Boys, Edmund John ameshajitoa katika mbio za ufungaji bora baada ya timu yake kutolewa na Angola baada ya kukubali kichapo cha 4-2.

Mchezaji yoyote ambaye atachukua ufungaji bora atazidi kujiweka katika sehemu nzuri ya maisha ya soka mbeleni.

WAFUNGAJI Osvaldo Pedro C (mabao 3 )

Edmund Johh (2)

Ubani Wisdom (2)

Seidou Ismaila (2)

Jabaar Ibraheem (2)

 Tawfik Bentayeb (2)

Momo Toure (2)

 Wengine wenye bao moja kila mchezaji ni; Olatomi Olaniyan 1,  John Alou Amoo Akinkunmi 1, John Kevin 1,Wamba Leonel 1, Goal Steve Mvoue 1, Aliou Balde 1, Samba Diallo 1, Ginea Bah Algassime 1, Kawooya Andrew 1, Asaba Ivan 1, Najib Yiga 1, Olakunle Olusegun 1 Goal Omary Omary 1 Goal Agiri Ngoda 1, Telson Tome 1, Davide Nzanza 1