Hospitali ya Mloganzila kuanza kutoa huduma Januari

Muktasari:

Akizungumza na vyombo vya habari katika ziara ya kutembelea eneo hilo  leo, Makamu Mkuu wa Chuo cha MUHAS, Ephata Kaaya alisema chuo hicho kinatarajiwa kudahili wanafunzi 15,000

Dar es Salaam. Ujenzi wa Hospitali na Chuo Kikuu cha Sayansi Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila umemalizika Agosti 31 mwaka huu na inatarajiwa kuanza kutoa huduma ifikapo Januari 2017.

Akizungumza na vyombo vya habari katika ziara ya kutembelea eneo hilo  leo, Makamu Mkuu wa Chuo cha MUHAS, Ephata Kaaya alisema chuo hicho kinatarajiwa kudahili wanafunzi 15,000.

"Jengo hili ni maalum kwa ajili ya kufundishia wataalamu wa masuala ya afya lakini pia litatoa huduma ya hospitali kwa wagonjwa mbalimbali na ina uwezo wa kulaza wagonjwa 571 pamoja na vyumba vya upasuaji 13," amesema Kaaya.