Ubelgiji yaing'oa Brazil, kucheza na Ufaransa Jumanne

Muktasari:

Hii ni mara ya kwanza kwa Ubelgiji kufikia hatua hiyo tangu 1986.

Moscow, Russia. Ubelgiji imeingia nusu fainali ya Fainali za Kombe la Dunia zinazoendelea Russia baada ya kuibanjua nje mabingwa mara tano Brazil kwa mabao 2-1, katika mechi kali.

Hii ni mara ya kwanza kwa Ubelgiji kufikia hatua hiyo tangu 1986.

Vijana wa Roberto Martinez walitawala kwa kiasi fulani mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa Kazan ikiwa ni ushindi wake wa tano mfululizo.

Brazil iliyoruhusu bao moja katika fainali za Russia ilifungwa bao baada ya kona ya Nacer Chadli kumbabatiza Fernandinho na kujaa wavuni katika dakika ya 10 ikiwa ni bao la nane la kujifunga katika fainali za mwaka huu

Fernandinho ambaye anacheza pamoja na Kevin De Bruyne Manchester City alimwadhiri baada ya kupiga kombora la umbali wa mita 20 lililojaa kwenye wavu wa Brazil baada ya kazi nzuri ya Romelu Lukaku.

 

Ubelgiji sasa itacheza na Ufaransa nusu fainali ambao waliwatoa Uruguay kwa kuwachapa mabao 2-0. Nusu fainali itachezwa St Petersburg Jumanne ijayo kuanzia saa 3:00 Usiku.