Ethiopia yasitisha safari za ndege za Boeing 737 Max
Muktasari:
- Ajali ya Ethiopian Airlines ni ya pili ya ndege aina hiyo chapa 737 Max 8 katika muda wa miezi mitano iliyopita
Ethiopia. Shirika la Ndege la Ethiopia limetangaza kusitisha safari za ndege zake zote za Boeing 737 Max 8 kuanzia jana Machi 10 hadi taarifa zaidi itakapotolewa.
Shirika hilo limeendelea kusema kwamba licha ya kuwa chanzo cha ajali hakijajulikana, wameamua kuchukua hatua hiyo kama tahadhari ya ziada.
Paia mkaguzi wa safari za ndege China ameagiza kampuni zote za ndege nchini China kusitisha safari za ndege aina hiyo ambayo ni ya muundo sawa.