Makocha wazawa kukutana Afcon fainali kwa mara ya kwanza katika miaka 21
Muktasari:
Rekodi zinaonyesha kuwa kocha aliyetwaa ubingwa huo mara nyingi ni Hassan Shehata wa Misri aliyetwaa mara tatu mfululizo na Charles Gyamfi wa Ghana, ambaye pia alitwaa mara tatu lakini si kwa miaka mfululizo.
Cairo, Misri (AFP). Fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika (Afcon) inayofanyika kesho Ijumaa baina ya Algeria na Senegal itakutanisha makocha wazawa kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 21.
Kocha Malgeria, Djamel Belmadi na Msenegali Aliou Cisse wote walikuwa wachezaji wa kiungo na ambao waliwahi kuchezea klabu za England.
Belmadi alipelekwa Manchester City kwa mkopo akitokea Marseille mwaka 2003 na baadaye alichezea Southmpton kwa misimu miwili, wakati Cisse alitumia muda wake mwingi za kusakata soka akiwa na klabu za Birmingham City na Portsmouth.
Cisse ana hamu kubwa ya kushinda mechi hiyo ya Cairo baada ya kushindwa kufunga penati katika fainali ya mwaka 2002 dhidi ya Cameroon na kuikosesha Senegal nafasi pekee ya kutwaa ubingwa hao walipofika fainali kwa mara ya kwanza.
Mara ya mwisho kwa fainali kukutanisha makocha wazawa ilikuwa mwaka 1998 wakati Misri, ikifundishwa na Mahmoud el Gohary, iliposhinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Afrika Kusini iliyokuwa inafundishwa na Ephraim 'Jomo' Sono jijini Ouagadougou.
Mjadala usioisha miongoni mwa watu wanaofuatilia soka la Afrika ni faida za makocha wazawa na wageni katika michuano hiyo umekuwa hausaidii kwa kuwa wageni wameshatwaa kombe hilo mara 16 wakati wazawa wametwaa mara 15.
Kocha Mmisri, Hassan Shehata anashikilia rekodi ya kwa kutwaa ubingw ahuo mfululizo mara tatu na Mghana Charles Gyamfi pia ametwaa tatu lakini si mfululizo.
Kocha mzaliwa wa Ufaransa, Herve Renard ndiye pekee ameshatwaa ubingwa huo akiwa na nchi mbili tofauti, akiiongoza Zambia mwaka 2012 na kurudia mafanikio hayo akiwa na Ivory Coast miaka mitatu baadaye.
Makocha waliotwaa ubingwa wa Afcon:
1957 Misri Mourad Fahmy (misri)
1959 Misri Pal Titkos (Hungary)
1962 Ethiopia Ydnekatchew Tessema (Ethiopia)
1963 Ghana Charles Gyamfi (Ghana)
1965 Ghana Charles Gyamfi (Ghana)
1968 Zaire Ferenc Csanadi (Hungary)
1970 Sudan Jirí Starosta (Czech)
1972 Congo Adolphe Bibanzoulou (Congo)
1974 Zaire Blagoje Vidinic (SRB)
1976 Morocco Gheorghe Mardarescu (Romania)
1978 Ghana Fred Osam-Duodu (Ghana)
1980 Nigeria Otto Gloria (Brazil)
1982 Ghana Charles Gyamfi (Ghana)
1984 Cameroon Radivoje Ognjanovic (SRB)
1986 Egypt Mike Smith (Wales)
1988 Cameroon Claude le Roy (Ufaransa)
1990 Algeria Abdelhamid Kermali (Algeria)
1992 I. Coast Yeo Martial (Ivory Coast)
1994 Nigeria Clemens Westerhof (Uholanzi)
1996 S. Africa Clive Barker (Afrika Kusini)
1998 Misri Mahmoud el-Gohary (Misri)
2000 Cameroon Pierre Lechantre (Ufaransa)
2002 Cameroon Winfried Schaefer (Ujerumani)
2004 Tunisia Roger Lemerre (Ufaransa)
2006 Misri Hassan Shehata (Misri)
2008 Misri Hassan Shehata (Misri)
2010 Misri Hassan Shehata (Misri)
2012 Zambia Herve Renard (Ufaransa)
2013 Nigeria Stephen Keshi (Nigeria)
2015 I. Coast Herve Renard (Ufaransa)
2017 Cameroon Hugo Broos (Ubelgiji)