Miradi ya Liganga, Mchuchuma yaiva, Serikali kuigawanya

Muktasari:

Serikali imetaja baadhi ya mambo ambayo yakikamilika yatasaidia kuanzisha mchakato wa kuanza kuchimba makaa ya mawe ya Liganga

Dodoma. Serikali imetangaza mpango wa kuanza uchimbaji wa makaa ya mawe ya Liganga ingawa bado kuna mlolongo wa mambo ambayo yameorodheshwa.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda ameliambia Bunge leo Jumatano Mei 14, 2019 akisema mipango yote ikiwemo ulipaji wa fidia ambapo wananchi watalipwa kabla ya mwaka wa fedha 2018/19 kuisha (Juni 30,2019).

Pia ametaja mambo mengi ambayo yanatakiwa kukamilishwa kabla ya kuanza kwa uchimbaji huo ambayo ni pamoja na kupitia mkataba na mwekezaji na kugawanya kwa mkataba usiwe Liganga na Mchuchuma ili kila mradi ujitegemee.

Mambo mengine ni ulipaji wa fidia,  umeme, ujenzi wa miundombinu na kupitia upya baadhi ya vipengele.

Kwa mujibu wa waziri, mkataba wa mwekezaji ulikuwa na vipengele ambavyo vingeitia hasara kubwa Serikali kama ingepitishwa kama ilivyo ikiwemo hasara ya dola 19.88 milioni kwa Liganga pekee.

Amesema kama mkataba ungepita kama ulivyo, aliyetia saini angefananishwa na Chifu Mangungo ambaye hutajwa kuwa aliingia mkataba mbovu na wakoloni akauza ardhi.