Serikali yapunguza kodi ya kampuni
Muktasari:
Uamuzi huo ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara
Dodoma. Katika juhudi za kuvutia uwekezaji nchini, Serikali imetangaza kupunguza kodi ya faida inayotozwa kwa kampuni kutoka asilimia 30 mpaka asilimia 20 ndani ya miaka mitano ijayo.
Punguzo hilo limetangazwa leo, Juni 14 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akiwasilisha bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19.
“Napendekeza kushusha kiasi cha (kodi ya faida) corporate tax kutoka asilimia 30 mpaka 20 ndani ya miaka mitano ijayo kuanzia 2018/19 mpaka 2022-23,” amesema Dk Mpango.
Uamuzi huo ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini ili kuvutia wawekezaji wa ndani na nje.
Soma Zaidi: Serikali yaongeza ushuru wa pipi, chokoleti