TBA yajisifu kuokoa Sh98 bilioni miradi yake saba

Muktasari:

Katika kipindi hicho pia TBA imepeleka gawiwo serikalini la Sh2 bilion, sawa na asilimia 15 ya mapato hayo.

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeokoa Sh 398 bilioni katika miradi saba iliyotekelezwa nchini katika mwaka wa fedha 2017/18.

Katika kipindi hicho pia TBA imepeleka gawiwo serikalini la Sh2 bilion, sawa na asilimia 15 ya mapato hayo.

Mtendaji Mkuu wa TBA, Elius Mwakalinga ameyasema hayo leo katika Maonyesho ya kimataifa ya biashara(Sabasaba) yanayoendelea jijini hapa.

Mwakalinga ameiitaja miradi hiyo saba  kuwa ni pamoja na wa Chuo Kikuu cha Dar es Salam uliogharimu Sh10bilioni badala ya Sh100bilioni  zilizopangwa hapo awali, ujenzi wa Ihungo uliogharimu Sh 12 bilioni  badala ya Sh108bilioni  na mradi wa ujenzi wa hospitali ya Geita uliojengwa kwa Sh17bilioni badala ya Sh 75 bilioni.

Aliutaja mradi mwingine kuwa ni ujenzi wa Hospitali ya Simiyu uliojengwa kwa gharama ya Sh12 badala ya sh47 bilioni.

Mwingine ni ujenzi wa hospitali ya Chato uliogharimu Sh13 bilioni badala ya 60, mradi wa nyumba za Magomeni uliogharimu Sh20bilioni badala ya Sh 86 bilioni, mradi wa Ukonga Sh10 badala ya 32.

“Wataalam wote hawa ni Watanzania,pia tunajivunia kwa kuwa na mitambo na vifaa  mbalimbali vya kisasa,pamoja na mtambo wa kuzalisha zege kwa mkoa wa Dodoma," amesema.