Mwana Mfalme apatikana na virusi vya Corona
London. Mwana Mfalme wa Uingereza Charles ambaye ndio Mrithi wa malkia Elizabeth amepatikana na virusi vya Corona, ofisi yake imesema leo Jumatano
Prince Charles ambaye ana umri wa miaka 71 yupo nchini Scotland na mke wake Camilla ambaye pia alipimwa hakuonekana kuwa na virusi hivyo vya COVID-19.
Katika taarifa nyingine kutoka Buckingham Palace inasema malkia mwenye umri wa miaka 93, ana afya njema na hajaonana mwanae huyo kwa majuma mawili.
"Ni kweli, Prince Charles amepimwa na amepatikana na virusi hivyo. Amekuwa akionesha dalili lakini ana afya njema na amekuwa akifanya kazi kutokea nyumbani kwa siku kadha zilizopita,” taarifa hiyo ilisema.
Kulingana na maelekezo ya serikali na ushauri wa kitabibu, Prince Charles na Mke wake wamelazimika kujitenga huko Scotland
Wanandoa hao walipimwa huko Aberdeenshire Kaskazini mashariki mwa Scotland, taarifa hiyo ilisema.