Papa apimwa corona

Muktasari:

  • Ni baada ya mmoja wa wasaidizi wake kugundulika na virusi vya corona.

Vatikani, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis amepimwa virusi vya corona (covid-19) na kuthibitika kuwa hajaambukizwa.

Papa Francis alipimwa virusi hivyo baada ya mmoja wa wachungaji anayeishi katika katika makazi yake kugundulika kuwa na corona.

Vyombo vya habari nchini Italia viliripoti kuwa mchungaji huyo ambaye ni ofisa wa sekretarieti ya jimbo aligundulika kuwa na virusi vya corona na kuzua hofu kuwa huenda Papa Francis naye ameambukizwa.

Kwa mujibu wa tovuti rasmi ya  Vatican, mchungaji huyo alikuwa mmoja wa washiriki wa karibu wa papa na sasa amelazwa katika Hospitalini ya Roma wakati idadi ya walioambukizwa katika jimbo hilo ikifikia watano.