Vifo vya corona vyafika sita Kenya

Muktasari:

Ni baada ya wagonjwa wengine wawili kufariki dunia leo.

Nairobi, Kenya. Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema kuwa watu wengine wawili wamefariki dunia kutokana na maambukizi ya virusi vya corona unasababisha ugonjwa wa Covid-19.

Rais Kenyatta ametangaza leo Jumatatu, Aprili 06 wakati akihutubia Taifa hilo.

Aisha, Rais Kenyatta ametangaza wagonjwa wengine wapya 16 waliopatikana mwishoni mwa wiki.

Rais Kenyatta alisema wagonjwa hao wapya wamefanya idadi ya maambukizi nchini humo kufikia 158.

Kufuatia hali hiyo Rais Kenyatta aliongeza zuio la safari za mafari ya umma yanayoingia jijini Nairobi yakitoka katika kaunti za Kilifi, Kwale na Mombasa ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huo.

Katika hatua nyingin, Rais Kenyatta alisema watu wanne wamethibitika kupona ugonjwa huo na kuruhusiwa kurejea nyumbani.