Anayetuhumiwa kumuua mfanyakazi wake afikishwa mahakamani
Muktasari:
- Mamia ya watu wamejitokea leo Alhamisi Machi 26, 2020 katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru kusikiliza kesi inayomkabili Mkami Shirima (30) anayetuhumiwa kumuua mfanyakazi wake wa ndani, Salome Zakaria(18) Machi 16, 2020.
Arusha. Mamia ya watu wamejitokea leo Alhamisi Machi 26, 2020 katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru kusikiliza kesi inayomkabili Mkami Shirima (30) anayetuhumiwa kumuua mfanyakazi wake wa ndani, Salome Zakaria(18) Machi 16, 2020.
Mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakama akiwa kwenye ulinzi mkali huku akiwa amefunikwa sehemu kubwa ya mwili wake.
Akisoma mashtaka yanayomkabili, wakili wa Serikali Penina Joachimu amesema alifanya mauaji hayo eneo la Mianzini jijini Arusha na kwamba upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kuomba mahakama kupanga siku nyingine ya kutajwa shauri hilo.
Hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, Amalia Mushi amesema kesi hiyo itatajwa tena Aprili 8, 2020 na mshtakiwa kurudishwa mahabusu.
Mshtakiwa huyo pia amesomewa kesi ya nyingine ya usafirishaji wa dawa za kulevya aina ya mirungi pamoja na Elias Lairien .
Hakimu mkazi wa Arusha Gwantwa Mwankuga ameahirisha a kesi hiyo hadi Aprili 8, 2020 kwa kuwa upelelezi haujakamilika.
Kesi hiyo ya kukutwa na mirungi ilitajwa kwa mara ya kwanza Septemba 24, 2019.