Majeruhi wengine wawili ajali ya moto Morogoro wafariki, idadi yafikia 97

Muktasari:

  • Idadi ya vifo vinavyotokana na ajali ya lori la mafuta ya petroli iliyotokea katika mtaa wa Itingi, Msamvu barabara ya Morogoro-Dar es Salaam nchini Tanzania, imefikia 97 baada ya majeruhi wawili waliokuwa wamelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH kufariki dunia.
  • Tangu ajali hiyo ilipotokea Jumamosi ya Agosti 10,2019, MNH ilipokea majeruhi 47 ambapo hadi leo Jumatatu asubuhi, waliobaki ni 18 ambao wamelazwa chumba cha uangalizi maalum (ICU).


Dar es Salaam. Majeruhi wawili kati ya 20 wa ajali ya lori la mafuta ya petroli lililoanguka kisha kuwaka moto waliokuwa wamelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam nchini Tanzania wamefariki dunia.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano MNH, Aminiel Aligaesha akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu Agosti 19,2019 amesema majeruhi waliobaki hospitalini hapo ni 18 ambao wote wapo kwenye chumba cha uangalizi maalum (ICU).

Amewataja waliofariki ni Rosijo Mollel (35) aliyefariki jana Jumapili mchana na Neema Chakachaka ambaye amefariki alfajiri ya leo Jumatatu.

Vifo hivyo viwili, vinafikisha idadi ya waliofariki kutokana na ajali hiyo kufikia 97.

 

Endelea kufuatilia Mwananchi kwa habari zaidi