Toleo jipya la iphone kuja Septemba mwaka huu

Hii inaweza kuwa habari njema kwa wapenzi wa simu kali zikiwamo Iphone.

Kwa mujibu wa Softbank kampuni inayojihusisha na utoaji huduma ya kimtandao ya nchini Japan imesema kuwa toleo lijalo la iPhone litatoka Septemba, kuanzia Septemba 20 mwaka huu.

Toleo la iphone mpya zitakuwa zimeendana na iliyotoka mwaka 2018 ambayo ni XS na XS Max ambazo zilitoka Septemba 21.