Mwili wa baba mzazi wa Mtume Mwingira kuzikwa baada ya siku 30

Muktasari:

Mazishi ya Elias Mwingira ambaye ni baba mzazi wa Mtume Josephat Mwingira yanafanyika leo Jumamosi Februari 22, 2020 Kibaha mkoani Pwani.

Kibaha. Mazishi ya Elias Mwingira ambaye ni baba mzazi wa Mtume Josephat Mwingira yanafanyika leo Jumamosi Februari 22, 2020 Kibaha mkoani Pwani.

Elias Mwingira alifariki dunia Januari 22, 2020 akiwa na umri wa miaka 94.

Ibada ya mazishi imeanza saa 4 asubuhi na kuhudhuriwa na watu wa kada mbalimbali akiwemo mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.

 

Endelea kufuatilia Mwananchi kwa taarifa zaidi