Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Minazi fursa iliyopewa kisogo nchini

Muktasari:

  • Zao la nazi pia hujulikana kama mti wa uzima kutokana na kuishi kwa muda mrefu. Kilimo cha minazi ni uwekezaji mkubwa kwa sababu mkulima anaweza kurithisha hata kizazi chake.

Zao la nazi pia hujulikana kama mti wa uzima kutokana na kuishi kwa muda mrefu. Kilimo cha minazi ni uwekezaji mkubwa kwa sababu mkulima anaweza kurithisha hata kizazi chake.

Kwa bahati mbaya, wakulima hawajaweza kutumia zao hilo ipasavyo kukuza uzalishaji wake na kuchangia uchumi wa nchi.

Katika hatua ya kuongeza uzalishaji, Serikali, kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (Tari), imeweka mikakati kadhaa ya kufufua shamba kongwe la minazi, kuboresha sekta hiyo na kusambaza mbegu ijulikanayo kwa jina la ‘the East African Tall’ kwa maeneo yote yanayoendesha kilimo cha nazi.

Aina hiyo mpya ya nazi ina uwezo wa kustahimili hali ya ukame na magonjwa hatari ya nazi na kupambana na wadudu waharibifu.

Meneja wa kituo cha Tari Mikocheni, Dk Fredy Tairo, anasema wakulima wanapaswa kujitosa katika kilimo cha mnazi au mti wa uzima, kwa sababu chochote kinachotokana na mnazi kinaweza kutumika.

“Ukianza na mnazi wenyewe hutoa mbao inayoishi kwa muda mrefu sana, majani yake yanatumika kuezekea nyumba, tumba la koko, mkeka, zulia na ganda la nazi mtu anaweza kutengeneza boli za kupikia, mkaa, nazi iliyokomaa inaweza kutumika kama kiburudisho na vitafunio kwa wakati mmoja,” alisema.

Aliongeza: “Tunawahimiza wawekezaji na wakulima wadogo kwa pamoja kutumia aina hiyo mpya ya mbegu (East African Tall variety) ili kuhakikisha wanaongeza thamani ya mazao, wakulima wengi wanalima zao la nazi na kulitumia majumbani kwa kupikia tu na kiasi kidogo kinatumika kuzalisha mafuta asilia.’’

Kilimo cha biashara

Kilimo cha nazi kina fursa ya biashara. Kinaweza kuchangia nakisi ya kitaifa ya mafuta ya kupikia, nazi ina uwezo wa kuchangia takriban asilimia 80 ya mafuta ya kula na kuziba pengo la uagizaji wake kutoka nje ya nchi.

Dk Tairo alisisitiza kwamba wameanzisha teknolojia mpya ya upatikanaji mafuta ambayo ni nyongeza ya thamani inayotumia mashine rahisi badala ya nazi inayouzwa kwa Sh400.

Kwa mujibu wa Dk Tairo, kupitia mashine hiyo nyepesi mkulima anaweza kuongeza thamani kwa kupata mafuta, ambapo ni ghali sana… Kwa mfano, ili kupata lita moja ya mafuta ya nazi asilia, inahitaji takriban nazi 20, ambazo ukibadilisha kwa thamani ya ufuatiliaji, ni karibu Sh8,000, lakini mkulima akiamua kuzalisha mafuta, lita moja inaweza kuuzwa kwa Sh40,000, hivyo kupata faida mara tano.

Tari tayari imeanza usambazaji wa teknolojia hizo kupitia vikundi vya wakulima, ambako ndiko Tari inakoelekea.

Tari pia imejikita katika upandaji wa zao hilo kwa ajili ya viwanda, kwani kwa sasa nchi inaagiza tui la nazi kutoka Thailand na Indonesia, kwa sababu hakuna uzalishaji wa kutosha ili kuendeleza viwanda hivyo, lakini kwa sasa kutokana na mipango ya kuanzisha shamba hilo katika kipindi cha miaka mitano hadi sita, wamejikita katika kilimo cha zao hilo, wataweza kukidhi malighafi ya sekta hiyo.

Zao la nazi ni kitegauchumi kikubwa kwa sababu mkulima anaweza kurithisha kizazi chake kwa sababu, kwa mfano, mkulima akiwa na umri wa miaka 25 baada ya miaka 70 anaweza kuwaachia watoto wake kuliendeleza.

Si hivyo tu, lakini pia Tari imeungana na mamlaka za ndani ili waweze kufanya kazi pamoja na kuongeza uzalishaji wa nazi. Lengo ni kwa wakulima wadogo na wakubwa wanaotaka kuanzisha mashamba makubwa ya minazi.

Alibainisha kuwa aina ya mbegu ya East Africa Tall huanza kutoa mavuno ikifikisha kati ya umri wa miaka mitano na sita, akisema uzalishaji wa kiuchumi hudumu kwa miaka 70.

Uzalishaji wa nazi

Hata hivyo, uzalishaji wa zao la nazi hivi karibuni umeshuka ikilinganishwa na hapo awali tulipokuwa na minazi takriban milioni 25 nchini. Eneo lililokuwa likizalisha minazi lilikuwa la hekta 265,000 ambazo zinaonyesha ni tani 800 za nazi nchini.

Kushuka kwa uzalishaji wa zao hilo kulichangiwa zaidi na changamoto za muda mrefu kama vile ukame, wadudu waharibifu na magonjwa hatari ya nazi ambayo ni tatizo kubwa na pia sekta hiyo kwa kipindi fulani ilisahaulika na kusababisha uzalishaji kushuka.

Sasa Tari, kwa kushirikiana na Serikali, inajitahidi sana kuhakikisha uzalishaji wa nazi unaongezeka au unaongezeka maradufu katika miaka mitano ijayo kutoka milioni 25 hapo awali.

Kwa kawaida, zao la nazi huhitaji udongo wa kichanga, udongo wenye kina kirefu unaoruhusu hewa na maji kupita na pia huhitaji mvua na ndiyo maana hustawi vizuri ufukweni na visiwani.

Kwa mujibu wa Dk Tairo, baada ya kufanya utafiti wa zao la nazi kwa miaka 25 nchini Tanzania walikuja na aina tatu kuu za nazi ziitwazo sub populations, lakini aina bora ya nazi iliyopendekezwa ni East African Tall inayoweza kustahimili hali kame na magonjwa hatari ya nazi, aina nyingine mbili za nazi, dwarf na hybrid, muda wao wa kuishi ni kati ya miaka 25 mpaka 30.

Lakini kwa sasa wanaweka nguvu katika uzalishaji wa aina ya nazi ya East African Tall kwa sababu inastahimili hali hizo.

Ukizungumzia na kuangazia zao la nazi, kimsingi ni zao lililokuwa likilimwa mwambao wa pwani kuanzia Tanga, Morogoro, Lindi, na Dar es Salaam pamoja na Mtwara, lakini kwa sasa kuna mikoa mipya yenye uwezo wa kulima zao hilo ikiwemo Mbeya hususan Kyela, Kigoma, Mwanza na Musoma,’’ anasema.