Gumzo kifo cha Profesa Benno Ndulu

Muktasari:

  • Gavana mstaafu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu amefariki dunia, akiacha gumzo la namna alivyofanikiwa kupangua kashfa ya uchotwaji wa fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow mwaka 2014.

Dar es Salaam. Gavana mstaafu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu amefariki dunia, akiacha gumzo la namna alivyofanikiwa kupangua kashfa ya uchotwaji wa fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow mwaka 2014.

Awali, aliingia ofisini mwaka 2008, akikutana na kashfa nyingine ya Akaunti ya Madeni ya Malipo ya Nje yaani `External Payment Arrears’ (EPA), iliyomhusisha mtangulizi wake, Dk Daudi Balali.

Profesa Benno Ndullu aliteuliwa kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Januari 2008 akimrithi Dk Balali.

Habari kamili jipatie nakala yako ya Mwananchi leo.