Magazeti yaliyofungiwa kuendelea kubaki kifungoni

Magazeti yaliyofungiwa kuendelea kubaki kifungoni

Muktasari:

  • Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ameelekeza televisheni za mtandaoni tu ndio zifunguliwe na sio vyombo vya habari vingine yakiwemo magazeti vilivyofungiwa kwa mujibu wa sheria.

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ameelekeza televisheni za mtandaoni tu ndio zifunguliwe na sio vyombo vya habari vingine yakiwemo magazeti vilivyofungiwa kwa mujibu wa sheria.

Ufafanuzi huo umetolewa leo Jumatano, Aprili 7 2021 na msemaji mkuu wa Serikali Gerson Msigwa kupitia ukurasa wake wa mtandao wake wa kijamii wa Twitter.

Ametoa ufafanuzi huo ikiwa imepita siku moja baada ya Rais Samia kuitaka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuvifungulia vyombo vya habari vilivyofungiwa huku akivitaka vyombo hivyo kufuata sheria.