Mahojiano ya mawakili, shahidi wa sita kesi ya kina Mbowe haya hapa!

Muktasari:

Jaji Joachim Tiganga kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na wenzake watatu wanaotuhumiwa kwa makosa ya ugaidi iliyokuwa ikiendelea katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.

Dar es Salaam. Jaji Joachim Tiganga kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na wenzake watatu wanaotuhumiwa kwa makosa ya ugaidi iliyokuwa ikiendelea katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.

Jaji Tiganga ameahirisha kesi hiyo baada ya shahidi wa sita wa upande wa mashtaka kutoa ushahidi na kuhojiwa na mawakili wa upande wa utetezi.

Leo Alhamisi Novemba 4, 2021 mahakama hiyo imepokea ushahidi wa upande wa mashtaka kutoka kwa shahidi wa sita.

Hapa ni sehemu ya mahojiano ya mawakili wa utetezi na shahidi huyo wa upande wa mashtaka

Baada ya kesi kuahirishwa kwa muda kwa mara ya tatu

Mahakama imerejea kwaajili ya upande wa utetezi kumuhoji shahidi

Mawakili wa pande zote mbili wako tayari


Wakili wa utetezi Jeremiah Mtobesya anaanza kumuhoji shahidi

Wakili: Unakumbuka uliwahi kuandika maelezo polisi kuhusiana na hiki

Shahadi: Ndio

Wakili: Ulikumbuka kuyasoma kukahakikisha ni sahihi

Shahidi: Ndio

Wakili: Unakumbuka ni tarehe ngapi?

Shahidi 23/3/2021

Wakili: Ni muda ulipita

Shahidi: Miezi 11

Wakili: Itakuwa sahihi nikisema wakati unaandika memori yako haikuwa sahihi

Shahidi: Sio sahihi

Wakili: Machi hadi leo miezi saba hukugundua namba ya jalada ilikuwa na tatizo

Shahidi: Nlikuwa naangalia jukumu nililopewa

Wakili: Unataka kusema content ya barua haikuwa na umuhimu

Shahidi: Nlikuwa najali jukumu nililopewa ndio maana nikasema kulikuwa na tatizo la kiuandishi

Wakili: Ulitaja mapungufu ya jalada kwenye barua yako

Shahidi: Sikumbuki

Wakili:  Naomba nipatiwe kielelezo halisi shahidi aweze kujikumbusha.

Wakili: Angalia hayo kama ni maelezo yako uliyoandika polisi

Shahidi: Ndio yenyewe

Wakili: Hebu Soma tusikie kama kuna maneno uliyosema

Shahidi: Katika maelezo hakuna sehemu yoyote iliyoandikwa

Wakili: Mwambie Jaji kama kuna sehemu yoyote kwenye kwenye maelezo yako

Shahidi: Kwenye maelezo hayapo

Wakili: Ulituonyesha

Shahidi: Utaratibu tukiletewa

Wakili: Ulituonyesha mfumo unavyofanya kazi

Shahidi: Sikuonyeshwa.

Mheshimiwa naomba kuishi hapo

Baada ya Wakili Jeremiah Mtobesya kumaliza kumuhoji shahidi sasa ni Wakili John Malya ameanza kumuuliza shahidi maswali

Wakili: Dhumuni la kufanya usajili wa silaha ni ili kuzuia uhalifu

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Unapofanya uchunguzi kwenye data base yako silaha ambayo haijasajiliwa kuna majibu inaleta

Shahidi: Inasema no record

Wakili: Hizo result umeleta mahakamani leo.

Shahidi: Kile nilichopresent ndio nilicholeta

Wakili: Wakati unaajiunga na Polisi ulikuwa na miaka 24 toka unaajiunga na Polisi umefanya zaidi ya miaka 24

Shahid: Ni sahihi

Wakili: Ulipoletewa uliuliza huenda ina tuhuma au la

Shahidi: Sikuuliza.

Wakili: Ni sahihi kili kilichosajiliwa ndio unachofanyia uchunguzi

Shahidi: Kama itakuwa imeingizwa kwenye mfumo

Wakili: Kwenye mazingira kama haya utajuaje kama namba zimefutwa

Wakili: Aina ya Silaha na mtengenezaji ndio tunaangalia

Shahidi: Kama zimefutwa nazo

Shahidi: Tunaangalia zile parameter tatu

Wakili: Umewahi kukutana na mazingira kama namba zimefojiwa

Shahidi: Tunaangalia zile

Wakili: Hiyo bunduki hukuletewa ni sahihi

Shahid: Sikufanya hivyo

Wakili: Unafanya kazi siku ngapi katika wiki

Shahidi: Saa 24 katika siku zote 7 za wiki


Wakili Mallya amemaliza sasa kaanza Wakili Fredrick Khiwelo

Wakili: Ni kweli tarehe 25 ulipokea barua kutoka kwa ASP Msangi

Shahidi: Kweli

Wakili: Mpo wa ngapi kwenye hicho kitengo

Shahidi: Tuopo 20


Wakili: Ulitoa taarifa ya umiliki au uchunguzi

Shahidi: Ndio

Wakili: Kwa mujibu wa maelezo yako ulitoa nini

Shahidi: Nilisema silaha haijasajiliwa

Wakili: Na wewe ulitakiwa kutoa nini

Shahidi: Inamilikiwa

Wakili: Ni sahihi kwamba mnafanyia uchunguzi siku hiyo hiyo mnapopokea barua

Shahidi: Ndio

Wakili: Wewe ulipokea barua tarehe 25 /11/2020 katoa majibu lini

Shahidi: 15 Machi 2021

Wakili: Ni Muda gani umepita

Shahidi: Miezi 5

Wakili: Je katika majukumu yako ulitaja jukumu lako la kutaja umiliki

Ni hayo tu Mheshimiwa.

Wakili Khiwelo amemaliza kumhoji shahidi na sasa anaanza Wakili Peter Kibatala.

Wakili: Kielelezo cha mashtaka namba 10 umetaja barua ya Tarehe 25 Novemba mwaka 2020 je ni sahihi kwamba barua hii ndiyo chanzo chote cha wewe Kuandika barua

Shahidi: Sahihi

Wakili: Ni sahihi kwamba bila barua hiyo wewe usingeandika hiyo barua

Shahidi: Ndiyo sahihi kabisa

Wakili: Sio kawaida yako kuandika tu barua

 Shahidi: Itakuwa

Wakili: Je hiyo Barua iliyokufanya uandike barua umekuja nayo

Shahidi: Sikuja nayo

Wakili:  Kwa ufahamu wako wewe ni muhimu au siyo huhimu

Shahidi: Kwa upande wangu sikuona umuhimu wa kuja nayo

Wakili: Kwa hiyo barua ndimo ambapo tungepata details za hiyo bunduki ambayo wewe ulipswa uifanyie uchunguzi

Shahidi: Sahihi kabisa

Wakili: Na Ndiyo humo tungeona Namba CZ 100, Callibre 9mm hatuwezi kuona popote zaidi ya hiyo barua

Shahidi: Sahihi kabisa

Wakili: Hujazungumza kabisa kuhusu CZ 100 9mm za ulikuwa unachunguza kwenye hiyo barua uliyoandikiwa na ni sahihi kabisa hujazunhumza kuhusu CZ 100, Callibre 09mm

Shahidi: Sahihi sikuzungumzia

Wakili: Na kuhusu electronic Data Base ulizungumza kuhusu mmiliki wa risasi

Shahidi: Kwenye electronic Data Base inaonyesha kuwa idadi ya risasi za kutumia wakati wa uhai wa leseni

Wakili: Ulitoa maelezo kwa Jaji kwanini hiyo Register hukuleta kama sababu ni nzito au kubwa

Shahidi: Sikutoa

Wakili: Unafahamu kwamba ushahidi wako lazima upitie sehemu kadhaa, Mahakama lazima ipime ushahidi wako

 Shahidi: Hiyo nafahamu

Wakili: Mwambie sasa Mheshimiwa Jaji kama ulifafanua kwanini ulishindwa kuleta extract ya negative result

Shahidi: Sikufafanua

Wakili: Nilisikia kwamba kuna typing error kwenye P10

Shahidi: Ndiyo

Wakili: Sasa Mahakama Itajuaje Kama hakuna tena makosa ya kibinadamu humu?

Shahidi:  Ni jukumu la Mahakama sasa kupima

Wakili: Unakubaliana na mimi kuwa akuna kosa linajitegemea kumiliki silaha bila kibali

Wakili: Swali langu la mwisho

Shahidi: Ndiyo

Wakili: Sheria inaitwaje

Shahidi: Inaitwa sheria ya Umiliki na Udhibiti wa silaha kifungu cha 20

Wakili: Kibatala Mheshimiwa Jaji ni hayo tu.

Wakili wa Serikali Piusi Hilla: Uliulizwa pia kuhusiana na silaha inayoingizwa nchini kutoka nje, wewe maelezo yako hayajaondoa possibility

Shahidi: Mfumo wetu wa silaha na usajili, mfumo wetu unamuimgiza mwishoni kabisa baada ya silaha imeshaingia nchini au kukamilisha utaratibu wa silaha itakwepo Kwenye Lisenced Private Warehouse

Wakili wa Serikali Mheshimiwa Jaji Mimi naishi hapo kam kuna wenzangu waendeleeeee Wakili wa Serikali wezangu na wao hawana


Jaji: Shahidi tunakushukuru unaweza kuendelea

Wakili Kidando: Mheshimiwa Jaji leo tulikuwa na shahidi mmoja tunaomba kuhahiriha shauri hili hadi kesho Novemba 5 saa tatu asubuhi.

Wakili Kibatala hatuna pingamizi Mheshimiwa

Jaji naahirisha kesi hii hadi kesho saa 3 nakuelekeza upande wa mashtaka kuleta mashahidi na washtakiwa wataendelea kubaki chini ya uwangalizi wa Magereza.

High Court iiiiiiiiiiiiii