Mwenyekiti Halmashauri Mufindi awaonya watendaji waliopewa pikipiki

Miongoni mwa pikipiki zilizotolewa na Halmashauri ya Mufindi mkoani Iringa kwa ajili ya maofisa watendaji kata kwa lengo la kuboresha utendaji wa kazi za kila siku. Picha na Mary Sanyiwa
Muktasari:
- Akizungumzia na Mwananchi leo Alhamisi Januari 26, 2023 Mgina amesema kuwa halmashauri hiyo ilitenga bajeti ya kununua pikipiki 27 yenye thamani Sh81 milioni ili kuwarahisishia utendaji wa kata kufanya kazi zao kwa urahisi katika ufuatilijia wa miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao kwa wakati.
Mufindi. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Festo Mgina wamewataka watendaji wa kata zote za halmashauri hiyo kuhakikisha wanatumia pikipiki walizogaiwa kwa malengo yaliyokusudiwa na watakaotumia kinyume watanyang'anywa pikipiki hiyo.
Akizungumzia na Mwananchi leo Alhamisi Januari 26, 2023 Mgina amesema kuwa halmashauri hiyo ilitenga bajeti ya kununua pikipiki 27 yenye thamani Sh81 milioni ili kuwarahisishia utendaji wa kata kufanya kazi zao kwa urahisi katika ufuatilijia wa miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao kwa wakati.
Aidha amesema kuwa pikipiki hizo ambazo zimegaiwa ni mali ya halmashauri hivyo mtendaji yoyote akipatika anafanya biashara ya bodaboda tofauti na matumizi ambayo yamekusudiwa hawatasita kuichukua na kupeleka sehemu nyingine kwa watendaji wa vijiji kwa sababu hawana usafiri huo.
"Hizi ni mali za Serikali hivyo wakizitumia vibaya hatutasita kuzichukua na kuwapa watu wengine kama watendaji wa vijiji ambao wanahitaji kwa kufuata kanuni zinazolinda mali za halmashauri kama ambavyo tunafanya kwa wakuu wa idara," Amesema Mgina.
Pia Mwenyekiti huyo amesema kuwa halmashauri hiyo umejipanga kununua pikipiki zingine 221 kwa ajili ya kuwagawia watendaji wa vijiji ili waweze kuteketeza majukumu yao kuwa urahisi.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kata ya Mninga, Ada Lwangiri ameshukuru halmashauri hiyo kwa kuwagawia pikipiki hizo jambo ambalo litawasidia katika utekelezaji wa majukumu yao.
"Tunaishuru halmashauri yetu kwa kutugawia pikipiki 27 kulinga na idadi ya kata kwa sababu zitatisaidia kurahisisha utendaji wetu hasa katika ufuatijia wa miradi ya maendeleo ambayo ipo kwenye kata na vijiji katika maeneo yetu pamoja na ukusanyaji wa mapato ya halmashauri hiyo," amesema Lwingiri.
Naye Afisa Mtendaji wa Kata ya Mdaburo Donald Mgaya amesema kuwa halmashauri imewasaidia kuwawezesha nyenzo muhimu ya usafiri wa pikipiki kwa sababu awali walikuwa wanapata changamoto kubwa ya umbali wa maeneo katika ufuatijia wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa.