Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mwili wa mwanzilishi wa Precision Air wawasili kijijini kwao

Mwili wa Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bodi ya kampuni ya shirika la ndege la Precision Air, Michael Ngaleku Shirima ukiwasili  jioni hii nyumbani kwake katika Kijiji cha Nayeme, Tarakea, Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro. Picha na Janeth Joseph

Rombo.  Mwili wa Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Shirika la Ndege la Precision Air, Michael Ngaleku Shirima umewasili katika Kijiji cha Nayeme, Tarakea, Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro.

Mzee Ngaleku alifariki usiku wa Juni 9, mwaka huu katika Hospitali ya Aghakan, Dar es salama alikokuwa amelezwa Juni 8 atazikwa kesho Juni 15 kijijini hapo katika makaburi ya familia.

Mwili huo umewasili kijijini kwake jioni hii ulipokelewa na mamia ya wananchi wakiwemo wafanyabiashara mashuhuri wa Mkoa wa Kilimanjaro, watawa wa kanisa Katoliki ambao wanahudumu katika kituo cha  kulelea watoto yatima cha Ngaleku kituo ambacho alikijenga Mzee Ngaleku pamoja na  viongozi wa chama na serikali wa mkoa huo.

Hata hivyo mwili wa mfanyabiashara huyo nguli wa  anga, umesindikizwa na viongozi mbalimbali wa serikali kutokea Jijini Arusha akiwemo Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Rombo, Profesa Adolf Mkenda, baadhi ya wabunge wa Bunge la Tanzania, wafanyabiashara mashuhuri nje na ndani ya Mkoa wa  Kilimanjaro pamoja na viongozi wengine waliokuwepo katika msafara huo.